UTAPENDA, SHEREHE ZA MWAKA MPYA WA KIISLAMU - BUMBWINI
Mjumbe wa Baraza la Maulamaa, Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Abdallah Haidar Abdullah, amewasihi wananchi wa Bumbwini kuendelea kuwa wamoja, kushikamana katika ibada na kumcha Mwenyezi Mungu kwa kuzingatia maamrisho na kujiepusha na makatazo yake ili kupata radhi na rehema zake. Sheikh Abdallah ametoa wito huo katika kongamano la kuadhimisha Mwaka Mpya wa Kiislamu lililofanyika katika Skuli ya Bumbwini, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Amesema vijana wanapaswa kuwa tayari kuyatekeleza mafundisho ya dini ya Kiislamu na kuishi kwa mujibu wa maadili mema, akieleza kuwa kufanya hivyo kutawasaidia kupata mafanikio duniani na Akhera. Aidha, amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na askari jamii kuendelea kuimarisha doria ili kudhibiti vitendo vya uhalifu vinavyohusishwa na matumizi ya dawa za kulevya na kulinda amani katika jamii. Kwa upande wake, Mkuu wa Dawati la Jinsia, Ndg. Machano Khamis, amesema dawati hilo lipo kwa ajili ya kulinda haki za wanawake, wanaume na watoto, huku akiitaka jamii kutoa taarifa kwa mamlaka husika mara tu vitendo vya ukatili au udhalilishaji vinapotokea. Nao waandaaji wa kongamano hilo, walimu wa vyuo vya madrasa, wamesema lengo la maadhimisho hayo ni kuhamasisha jamii kuthamini Mwaka Mpya wa Kiislamu, kuimarisha maadili ya dini na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kudumisha amani, umoja na mshikamano nchini. #Zanzibar #MwakaMpyaWaKiislamu #Bumbwini #MuftiZanzibar #Amani #Maadili #AsamOnlineTV #TrendingNow

MAPOKEZI YA RAIS WA ZNZ LUSHOTO TANGA MAULID IRSHAAD

DC LAILAH AKAMATA WAYA ZA UMEME ZILIZOIBIWA BUMBWISUDI

MARIDHIANO YA CCM NA ACT YATAJWA KUWA CHACHU YA UMOJA NA MAENDELEO ZANZIBAR

Cooking A Massive Lamb Pilaf For a Mountain Village Feast!

Argentina vs. Egypt Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau

RASMI KIZIMKAZI FESTIVAL 2026 KUFANYIKA AGOSTI 12

MBUNGE PONDEZA AJITOSA KUMSAIDIA KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI

SABA SABA YASHEREHEKEWA KWA AMANI NA UTULIVU - ZANZIBAR

MHE. HEMED AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA RC MJINI MAGHARIBI

KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI AANZA MATIBABU

UMOJA WA WANAZUONI WA KIISLAMU TANZANIA WALAANI KITENDO CHA KUDHALILISHWA SHEIKH NURDEEN KISHK

خطبتي و صلاة الجمعة من المسجد النبوي الشريف بالمدينة المنورة - 1448/01/18هـ

PROFESSOR KITILA MKUMBO CALLS FOR A NEW CONSTITUTION | CLAIMS THE CURRENT ONE IS FOR A SINGLE-PAR...

DC LAILAH AAGIZA BI. AZIZA AKAMATWE KWA TUHUMA ZA KUHUJUMU MAJI - MTOFAANI

SHEIKH MSELEM BIN ALI HUD 42 - 49 MASJID SAHABA MTONI KIDATU ZANZIBAR

"KUMEKUCHA"UST MAZINGE TAJIRI HAROGWI...IMAMU WA SHEKILANGO ATOA NASAHA NAYE

KISAUNI YAACHANA NA KERO YA BARABARA MBOVU

MAMA MPAKISTAN ACHANGIWA MILLION 7 |NATAKA KUJENGA NIWALEE WANANGU

HIKI NDICHO KINACHOJIRI MUDA HUU TANZANIA MAANDAMANO YA SABA SABA

