MBUNGE PONDEZA AJITOSA KUMSAIDIA KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI
Mbunge wa Jimbo la Chumbuni, Mhe. Ussi Salum Pondeza, amemtembelea kijana Juma Mkuya Juma, ambaye anakabiliwa na changamoto ya kupooza mwili baada ya kupata ajali alipokuwa akipiga makwachu katika Bahari ya Maruhubi, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi. Akizungumza na ASAM Online TV, Mhe. Pondeza amesema yuko tayari kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha Juma anapata matibabu stahiki na kurejea katika hali nzuri ya afya. Ameeleza kuwa hatua za awali zitaanza kwa kumpatia huduma za kitabibu kupitia Kliniki ya Hospitali ya Wilaya ya Lumumba kwa ajili ya uchunguzi na tathmini ya afya yake, kabla ya kuendelea na matibabu yanayohitajika. Kwa upande wake, mama wa Juma, Bi. Ashura Juma, amemshukuru Mbunge Pondeza kwa moyo wa kujali na kufuatilia hali ya mwanawe, akisema hatua hiyo imeirejeshea familia yao matumaini mapya. Naye Juma Mkuya Juma ametoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Chumbuni pamoja na mwakilishi wa eneo hilo kwa kumtembelea na kuonesha dhamira ya kumsaidia kupata matibabu. Aidha, kijana anayehamasisha upatikanaji wa wafadhili kwa ajili ya matibabu ya Juma amesema anaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha msaada unaohitajika unapatikana na kumrejeshea Juma matumaini ya kuendelea na maisha yake. #ASAMOnlineTV #Zanzibar #Chumbuni #JumaMkuya #Afya #Msaada #Habari #News #Community #FYP #ForYou #Trending #TikTokTanzania #Viral #Hope #TogetherWeCan

Mzee wa miaka 99 afia gerezani na ujumbe kwa Rais Samia | GUMZO MAALUM | Sheikh Ponda & M.Ghassani

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST

ITAKULIZA... TAZAMA WAZIRI MKUU AKIWAPAMBANIA Wananchi Kesi zao Mara

DC LAILAH AAGIZA BI. AZIZA AKAMATWE KWA TUHUMA ZA KUHUJUMU MAJI - MTOFAANI

Cooking A Massive Lamb Pilaf For a Mountain Village Feast!

MPASUKO CHAUMMA: MABILIONI YAMNG'OA SALUM MWALIMU, APISHA UCHUNGUZI

RC MJINI MAGHARIBI ATAKA WALIOHUSIKA NA VURUGU DARAJANI WAJISALIMISHE

Wagonjwa wa Gaza wahangaika kupata matibabu licha ya vita kusitishwa. Katika Dira ya Dunia TV.

EXCLUSIVE: JAMES MBOWE AIVAA CHADEMA "WAMEACHA SIASA WANAFANYA HARAKATI"

MAMLAKA YA USAFIRI NA USALAMA BARABARANI ZANZIBAR YATANGAZA ADA NA TOZO MPYA 108

KISAUNI YAACHANA NA KERO YA BARABARA MBOVU

ZFDA YABAINI ZAIDI YA TANI 1.5 ZA BIDHAA ZILIZOHARIBIKA KWENYE GHALA LA CROSS BOARDES

ZFDA YATEKETEZA BIDHAA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI, SOSEJI, NYAMA NA MAFUTA

LIVE:WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA ANAZUNGUMZA NA WANANCHI WA IGOWOLE

YOU Won’t Believe This 😱 Homeless 8 Years of Hair & Beard Transformation

"Soon u won't be a president's Son.." Akena Obote wonders why a 27th in hierarchy control everything

🔴TAARIFA YA HABARI, SAA MBILI JULAI 03, 2026 -MAONESHO YA SABA SABA YAZINDULIWA RASMI DAR E S SALAAM

ATIWA MBARONI KWA KUWANYIMA WANANCHI HUDUMA

ZBS YAMJENGEA NYUMBA BI. BIHALIMA

