KISAUNI YAACHANA NA KERO YA BARABARA MBOVU
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara ili kurahisisha usafiri, kuunganisha maeneo mbalimbali na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Wananchi wa Kisauni wameeleza kufurahishwa na ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita tatu kutoka Kisauni Mkunazi Samaki hadi Kwarara kwa Ngurangwa, wakisema mradi huo umeondoa changamoto ya muda mrefu iliyokuwa ikiwakabili kutokana na ubovu wa barabara hiyo. Wamesema kukamilika kwa barabara hiyo kutarahisisha usafiri wa wananchi, usafirishaji wa mazao pamoja na upatikanaji wa huduma muhimu, hatua itakayochangia kukuza uchumi wa eneo hilo. Akizungumza kuhusu mradi huo, Msimamizi wa Barabara kutoka Wakala wa Barabara Zanzibar (ZANROAD), Suleiman Issa Suleiman, amesema Serikali iliamua kutekeleza ujenzi huo baada ya kutambua umuhimu wa barabara hiyo na changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi. Ameongeza kuwa mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuendelea kuboresha miundombinu ya usafiri ili kuinua maisha ya wananchi na kuharakisha maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar. #ASAMOnlineTV #Zanzibar #ZANROAD #Barabara #Miundombinu #Maendeleo #Kisauni #Habari #News #FYP #ForYou #Trending #TikTokTanzania #Viral #Infrastructure

WAZANZIBAR SIO WABAGUZI - DK MUCHUNGUZI, AFUNGUKA MAZITO

MAKALA YA MABORESHO YA BANDARI YA MALINDI

🔴#LIVE: WAZIRI MKUU ANAFUNGUKA MAZITO MUDA HUU/YUDA NA ISHU YA SABASABA

MBUNGE PONDEZA AJITOSA KUMSAIDIA KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI

Rais Mwinyi leo amtumbua Mkurugenzi wa ZRB

DKT. SAADA : ZANZIBAR HAIWEZI KUBEBA MATIBABU YA WATU MILIONI 60, KAULI YANGU IMEPOKELEWA KISIASA

MJI MKONGWE YAVUNJA UKIMYA, YATOA ONYO KALI KWA WAVUNJIFU WA SHERIA

DC LAILAH AAGIZA BI. AZIZA AKAMATWE KWA TUHUMA ZA KUHUJUMU MAJI - MTOFAANI

ALI KARUME: MFUMO WA SERIKALI 3 NDO UNAFAA, WE RAIS MZIMA WA ZANZIBAR ANAKUWA WAZIRI KWENYE MUUNGANO

MAMLAKA YA USAFIRI NA USALAMA BARABARANI ZANZIBAR YATANGAZA ADA NA TOZO MPYA 108

MANISPAA YA MJINI ZANZIBAR YATOA AGIZO LA KUONDOA WAFANYABIASHARA WASIORASMI

WANA TANGA KUNUFAIKA NA MRADI WA EACOP

MWAFAKA WAIVA ZANZIBAR,SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA (SUKI) MBIONI KUREJEA

🔴TAARIFA YA HABARI, SAA MBILI JULAI 03, 2026 -MAONESHO YA SABA SABA YAZINDULIWA RASMI DAR E S SALAAM

ZBS YAMJENGEA NYUMBA BI. BIHALIMA

MAMLAKA YA MJI MKONGWE YAWABANA WAFANYABIASHARA HOLELA DARAJANI

Unbelievable Smart Worker & Hilarious Fails | Construction Compilation #5 #adamrose #smartworkers

ZIARA YA KIMICHEZO BAINA YA CHUO CHA MAFUNZO ZANZIBAR NA MAGEREZA TANZANIA

Worst Plane Landing Fails Caught on Camera

