SABA SABA YASHEREHEKEWA KWA AMANI NA UTULIVU - ZANZIBAR
Wakati wafanyabiashara wakiadhimisha Siku ya Sabasaba, baadhi yao wamesema jambo kubwa linalowapa faraja ni kupata fursa ya kufanya biashara kwa uhuru katika eneo jipya walilotengewa, wakieleza kuwa hatua hiyo imeanza kuvutia wateja na kuongeza matumaini ya kukuza biashara zao. Wakizungumza na Asam Online TV, wafanyabiashara hao wamesema wanaridhishwa na mazingira ya eneo hilo, wakiamini kuwa yataongeza ufanisi wa shughuli zao na kuwapa nafasi nzuri ya kuendeleza biashara zao kwa utulivu. Hata hivyo, wameiomba Serikali kutatua changamoto zinazowakabili, hususan ukosefu wa huduma ya umeme, wakisema upatikanaji wa huduma hiyo utachochea zaidi ukuaji wa biashara na kuongeza mapato yao. Kwa upande wake, Mjumbe wa Kamati ya Ugawaji wa Nafasi katika eneo la Garden, Said Ali Suleiman, amesema changamoto zilizobaki zipo katika hatua za kushughulikiwa, huku akiahidi kuwa mamlaka husika zinaendelea kutafuta suluhisho la kudumu kwa manufaa ya wafanyabiashara wote. Wafanyabiashara hao wameeleza matumaini yao kuwa maboresho yanayoendelea kufanyika, ikiwemo upatikanaji wa huduma ya umeme, yataongeza fursa za biashara na kuchangia maendeleo ya uchumi wao pamoja na jamii kwa ujumla. #Zanzibar #Sabasaba #Biashara #Garden #Wafanyabiashara #AsamOnlineTV #TrendingNow

MHE. HEMED AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA RC MJINI MAGHARIBI

DC LAILAH AKAMATA WAYA ZA UMEME ZILIZOIBIWA BUMBWISUDI

MAAJABU YA BANDARI YA MPIGA DURI MAKAMO WA PILI WA RAIS AFIKA KUKAGUA

SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU WA VIUNGO

MAJENGO YA KIHOSTORIA YAENDELEA KUKARABATIWA ZANZIBAR

DC LAILAH AAGIZA BI. AZIZA AKAMATWE KWA TUHUMA ZA KUHUJUMU MAJI - MTOFAANI

MAKAMU WA PILI WA RAIS ASEMA SASA FIDIA ZILIPWE

UTAPENDA, SHEREHE ZA MWAKA MPYA WA KIISLAMU - BUMBWINI

SMZ KUENDELEA KUIMARISHA VIWANJA VYA NDEGE KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Ushqim hallall midis Spilles: Piceria Tani dhe Hotel Medina- RTI

🔴LiVE:SIMANZI: MAYELE AUWA WAWILI IGOMBE-MWENYEKITI AFARIKI JIRANI AHUSISHWA

KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI AANZA MATIBABU

MBUNGE PONDEZA AJITOSA KUMSAIDIA KIJANA WA MAKWACHU ALIYEPOOZA MWILI

ZFDA YATEKETEZA BIDHAA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI, SOSEJI, NYAMA NA MAFUTA

KISAUNI YAACHANA NA KERO YA BARABARA MBOVU

UNDP YAKABIDHI BAJAJI 14 KWA SERIKALI YA ZANZIBAR

HABARI KUBWA JIONI HII KUTOKA TANZANIA...

Zanzibar Fish & Chips... Made the Traditional Way! 🇹🇿🍟

በቀን 17 አስክሬን ወደ ኢትዮጵያ ተልኳል.... የመጤ ጠል ችግር በደቡብ አፍሪካ መጨረሻዉ ምንድነዉ ከፓስተር ዶ/ር ሳሙኤል ጌታቸዉ| Seifu on EBS

