MARIDHIANO YA CCM NA ACT YATAJWA KUWA CHACHU YA UMOJA NA MAENDELEO ZANZIBAR
Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima (AAFP), Said Soud Said, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika kuimarisha maridhiano kati ya CCM na ACT Wazalendo, akieleza kuwa hatua hiyo inaonesha dhamira ya viongozi wa vyama hivyo katika kuendeleza amani, umoja na maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi Ndogo ya AAFP, Mwera, Wilaya ya Magharibi "A", Mkoa wa Mjini Magharibi, Said amesema lengo kuu la maridhiano hayo ni kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na amani, utulivu na mazingira wezeshi yatakayochochea maendeleo ya wananchi pamoja na ustawi wa taifa. Ameeleza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo katika sekta mbalimbali, hivyo kuna umuhimu kwa wananchi kuendelea kuilinda na kuunga mkono juhudi zinazolenga kuimarisha mshikamano wa kitaifa. Aidha, amempongeza Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Mhe. Othman Masoud Othman kwa hatua ya kufanikisha maridhiano hayo, akisema yameonesha uzalendo na dhamira ya dhati ya kuweka mbele maslahi ya Zanzibar na wananchi wake. Said ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuwaunga mkono viongozi hao kwa kudumisha amani, umoja na mshikamano, akieleza kuwa hali hiyo itasaidia kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na kuijenga Zanzibar yenye ustawi na mafanikio kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

PROFESSOR KITILA MKUMBO CALLS FOR A NEW CONSTITUTION | CLAIMS THE CURRENT ONE IS FOR A SINGLE-PAR...

UJENZI WA BARABARA YA MALAWI–KINAZINI KUANZA JULAI 10 KUBORESHA USAFIRI ZANZIBAR

INAUMIZA, MAMA ALIYEPATA WATOTO WAWILI PEKEE KWA SHIDA NA KUFARIKI GHAFLA SIKU MOJA, ASIMULIA

How Rwandan Refugees SECRETLY Built a Rebel Movement in Uganda & Kenya | Tharcisse Karugarama

Rais Trump asema leo usiku Marekani itaishambulia vikali Iran. Katika Dira ya Dunia TV.

LISSU ATEMA NYONGO | 'SITOKUBALI UHUNI, NA SITAHAMA CHADEMA LABDA NIFE AU NIFUKUZWE'

Show Me The 300 Jobs You Created After 300 Ghanaians Left! | Julius Malema

Full Donald Trump NATO press conference: President addresses Iran war, tariffs and AI

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST

This Is What Brexit Cost the World

Trump Meddles in USA World Cup Game & America's 250th Takes a Nosedive | The Daily Show

KUMEKUCHA ACT WAZALENDO WAPASUA UKWELI KUELEKEA MARIDHIANO

MBETO AFICHUA KILICHOJIRI KWENYE MAZUNGUMZO YA CCM NA ACT VIPENGELE 9

MHE. HEMED AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA MAMA MZAZI WA RC MJINI MAGHARIBI

'Downright addled and CRAZY': Nicolle reacts to Trump's UNHINGED outbursts at NATO summit

WENGI HAWAJUI! Sababu za Mashambulizi Mapya na Machafuko Mashariki ya Kati / Sheikh Shabani Afafanua

DW Kiswahili Habari za Ulimwengu | Podcast | Dunia Yetu | Leo Mchana | 08.07.2026 | Swahili News

Dkt. Ananilea Nkya atoa tahadhari Umoja wa Tanzania.

KISAUNI YAACHANA NA KERO YA BARABARA MBOVU

