TUHUMA ZA UCHUKUAJI NYETI WAENDELEA KULETA HOFU NDANI YA JAMII...

KATAVI: Taharuki yaendelea kutanda katika manispaa ya Mpanda mkoani Katavi baada ya tuhuma za wanaume wawili katika soko linalofahamika kwa jina la Kababaye kudaiwa kuguswa bega na nyeti zao kutoweka. Hali hiyo imeendelea kuleta hofu ndani ya jamii ambapo wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo ambalo linaendelea kukwamisha shughuli za watu. Aidha wananchi wamesema imani za kishirikina ndizo zinachangia kuleta taharuki hiyo ambapo jamii imeaswa kutoamini viashiria vyovyote vya imani za kishirikina.