WACHIMBAJI WALIA NA WAZIRI....

KATAVI: Wachimbaji wa madini mkoani Katavi wamelalamikia kuwepo kwa utitiri wa leseni katika maeneo ya uchimbaji ambapo Yassin Katempa ambaye ni mwenyekiti wa wachimbaji mkoani humo na Anna Lupembe ambaye ni mbunge wa jimbo la Nsimbo wamesema ni kero kwa wachimbaji wadogo. Waziri wa madini Antony Mavunde amechukua maamuzi ya kufuta leseni zote za wachimbaji hii leo tarehe 12/05/2026 huku akisisitiza utoaji leseni kwa njia ya kisasa ambayo itahakikisha inaondoa kero za namna hiyo.