KATAVI: TAZAMA VIDEO MWANAFUNZI wa DARASA la SABA ANUSURIKA KUOLEWA KIMILA

The Katavi Independent || Taasisi isiyo ya Kiserikali Usevya Development Society (UDESO) imemnusuru binti (Jina limehifadhiwa) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la Saba katika shule ya msingi Maimba Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi baada ya kutaka kuozeshwa kimila kwa kutumia nguvu. Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Eden Wayimba mapema Jana Juni 30, 2023 majira ya saa Tano asubuhi katika Kijiji cha Itula alitibua mipango hiyo baada ya kukutana na kundi la wavulana wakiwa wamemshikilia binti huyo katika harakati za kumtorosha. "Ni kweli tumemuokoa binti huyo majira ya asubuhi baada ya kukutana na kundi la Vijana ambaox, na tayari tumemkabidhi kwa Mtendaji wa Kata ya Chamalendi akiwa salama" -Amesema Mkurugenzi wa Taasisi hiyo. Kwa upande wake binti huyo amesema anahitaji kusoma sio kuolewa na kuwa hapendi mila hiyo ya kuwalazimisha watoto wadogo kuolewa. Imebainika, katika vijiji vya Kashishi na Itula kumekuwa na wimbi la mabinti wadogo kuozeshwa kimila kwa kutumia mila ya Chagulaga ambapo imekuwa ikitumiwa na jamii ya kifugaui. Mila ya Chagulaga ni mila inayoendekezwa na jamii hiyo ya wafugaji ambapo Vijana wadogo wamekuwa wakijikusanya sehemu moja na pale binti anapokatiza maeneo hayo wanamkimbiza na kumpiga fimbo na yule atakayewahi kumkamata basi binti huyo huwa mke wake. Juhudi za kuwatafuta Viongozi wa eneo hilo zinaendelea ili kufahamu ukweli kuhusu tukio hilo na jitihada za kukomesha Chagulaga.