BIBI MLEMAVU ATATULIWA KERO YAKE

KATAVI: Bibi mlemavu wa macho ajulikanaye kwa jina la Adela Mlela mkazi wa manispaa ya Mpanda mkoani Katavi ametoa malalamiko yake ya kuvamiwa eneo lake lenye hekali zaidi 60 ambalo limevamiwa na wachimbaji. Bibi huyo amesema eneo lake hilo lina madini ambapo ameimba kupewa fidia au maeneo yake hayo wayanunue kwa utaratibu maalum Afisa madini mkoa wa Katavi Andrew Mwalugaja amesema eneo hilo analitambua ambapo mara kadhaa amekua akitafuta njia bora ya bibi huyo kunufaika na eneo lake. Waziri wa madini Antony Mavunde ameagiza ndani ya siku saba kuanzia hii leo 12/05/2026 kutatua kero hiyo ili bibi huo apate haki yake haraka.