WAZAZI WAONYWA KUONGEZA ULINZI WA WATOTO BAADA YA VIFO VYA WATOTO WATATU KWA KUZAMA
Wazazi na walezi Zanzibar wametakiwa kuongeza uangalizi kwa watoto wao na kuhakikisha hawafiki katika maeneo hatarishi bila usimamizi, kufuatia vifo vya watoto watatu wenye umri wa miaka 12, 13 na 15 waliofariki kwa kuzama katika bwawa lililopo Mbuzini, Wilaya ya Magharibi "A", Julai 13 mwaka huu. Akizungumza wakati wa kuwafariji familia zilizopoteza watoto hao huko Mbuzini, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar, Mhe. Anna Athnas Paul, amesema tukio hilo ni pigo kubwa kwa jamii na limetoa funzo la umuhimu wa wazazi na walezi kuwa karibu na watoto wao wakati wote ili kuwakinga na ajali pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuhatarisha maisha yao. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar, Makame Khatib Makame, amesema kamisheni hiyo itaendelea kutoa elimu mashuleni na katika jamii kuhusu mbinu za kujikinga na majanga, ikiwemo hatari ya kuzama, ili kupunguza matukio ya aina hiyo. Naye Mkuu wa Wilaya ya Magharibi "A", Lailah Burhan Ngozi, amewataka wananchi kuacha uchimbaji holela wa mchanga unaosababisha kuwepo kwa mabwawa makubwa yanayohatarisha usalama wa watoto na wananchi kwa ujumla. Viongozi hao wamewataka wananchi kushirikiana kuondoa mazingira hatarishi, kuongeza ulinzi wa watoto na kuchukua tahadhari ili kuzuia matukio kama hayo yasijirudie.

TUKIO LA KUSIKITISHA: KIJANA AKUTWA AMEFARIKI MAGOGONI

Pwani: Maji ya bahari yaendelea kusonga na kuingia katika makazi ya watu Kilifi na Lamu

Family Demands Answers After Grade 10 Student Dies Following Fight at Thika High School

The Baby Stealers - BBC Africa Eye Documentary

DC SAID HAJI MRISHO AKAGUA KARO LINALOVUJISHA MAJI MACHAFU FORODHANI

SIMANZI BUBUBU: VIJANA WATATU WAFARIKI KWA KUZAMA KATIKA MTO MWANAMANJAA

YEESOZZE EKIKAJJO NE BAKYOOKYA, BAMUKUBA NE BAMUTTA, AVUDDEYO NE BAMUKUBA NE BAMUTTA

Torrential Rainfall Floods Communities In Lekki, Ajah, Ibeju-Lekki

Maalin-dhan Ayaan Deegaanka Jazeera ku noolaa.

ስነ ስርዓት ምምራቕ መበል 38 ዙርያ ኣባላት ሃገራዊ ኣገልግሎት - ሳዋ | ERi-TV

UKWELI HUU HAPA! HALI YA MWENGE JIJINI DAR ES SALAAM NA MOROGORO JUU YA SIKU HII YA SABABASA

MTANZANIA PEKEE KWENYE MAZISHI YA KHAMENEI | AMEKUFA HANA HATA GARI AMEZIKWA NA WATU MILIONI 42

The Most Important Country in Africa You’ve Never Heard Of (Djibouti 🇩🇯)

RC MJINI MAGHARIBI AAGIZA KUFUTWA KWA VIBALI VYA UJENZI NDANI YA HIFADHI ZA BARABARA

Trump Gives Medical Assessment of Graham's Death, Backs Down on Strait of Hormuz Toll: A Closer Look

UJENZI WA BARABARA YA MALAWI–KINAZINI KUANZA JULAI 10 KUBORESHA USAFIRI ZANZIBAR

How Rwandan Refugees SECRETLY Built a Rebel Movement in Uganda & Kenya | Tharcisse Karugarama

ZAIDI YA MILIONI 200 KUTUMIKA KATIKA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA LA TAWI LA CCM - JANG'OMBE

🔴#Live:MAMA FATMA AIBIWA PESA YA NAULI! MASWALI MAGUMU KUHUSU AJENT,MKATABA NA HAKI ZA WAFANYAKAZI..

