PSSSF YAENDELEA KUTOA FURSA ZA AJIRA KWA WANANCHI

Katika maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), PSSSF Tanzania inaendelea kuonesha mchango wake katika maendeleo ya Taifa kupitia uwekezaji wenye tija. Uwekezaji wa PSSSF katika Nguru Hills na Kilimanjaro Leather umechangia kuchochea ukuaji wa uchumi, kuongeza thamani ya rasilimali za ndani, na kuunda fursa za ajira kwa Watanzania. PSSSF inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuwekeza kwa manufaa ya wanachama na maendeleo endelevu ya Taifa.