MAMLAKA YA USAFIRI NA USALAMA BARABARANI ZANZIBAR YATANGAZA ADA NA TOZO MPYA 108

Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani Zanzibar imetangaza rasmi ada na tozo mpya 108, hatua inayolenga kuboresha utoaji wa huduma na kuongeza ufanisi katika sekta ya usafiri na usalama barabarani. Akizungumza wakati wa kutangaza mabadiliko hayo, Mwanasheria wa Mamlaka hiyo, Hassan Vuai Hassan, amesema marekebisho ya ada na tozo hizo yamefanyika baada ya kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kuhakikisha viwango vipya vinazingatia hali halisi ya wananchi pamoja na mahitaji ya utoaji wa huduma. Amesema baadhi ya mabadiliko hayo yanahusisha ongezeko la ada ya fomu kutoka shilingi 2,000 hadi shilingi 10,000, marekebisho ya ada za wanafunzi wa udereva pamoja na leseni za vyombo vya moto vya magurudumu mawili. Aidha, amesema hatua hiyo inalenga kuboresha huduma zinazotolewa na mamlaka, kuimarisha usalama barabarani na kuhakikisha mfumo wa utoaji wa huduma unaendana na mahitaji ya sasa. #Zanzibar #Usafiri #UsalamaBarabarani #AdaMpya #Huduma #AsamOnlineTV #TrendingNow