Tunataka tuifanye Morogoro liwe Jiji - RC Malima.

Serikali Mkoani Morogoro ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima imedhamiria na inaendelea kuweka mikakati na mipango madhubuti kuhakikisha Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro inakuwa miongoni mwa Miji mikubwa hapa Nchni. Hayo yamebainishwa Julai 2, 2024 na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Adam Kighoma Malima wakati wa kikao Maalum cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika mkoani humo. Mhe. Malima amesema kupitia ujio wa reli ya kisasa ya mwendo kasi (SGR) inakuwa chachu ya maendeleo katika Mkoa huo na itachangia kwa vikubwa Mkoa wa Morogoro kuwa jiji kwa sababu ya uwepo wa wasafiri wengi wanaopita mkoani humo ambao wataongeza mzunguko wa fedha na Halmashauri kujipatia mapato ya kutosha. "...sasa nyie mkitaka kujiita city village ni nyie lakini mimi nataka Morogoro iitwe city council.." amesisitiza Mhe. Adam Malima. Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amesema, Halmashauri hiyo haiwezi kuwa jiji kama ukusanyaji wa mapato ya ndani ni hafifu, pamoja na kuipongeza kuwa ndiyo Halmashauri inayoongoza kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani kati ya Halmashauri zote za Mkoa huo, bado ameitaka Halmashauri hiyo kuweka mikakati ya kuongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa dhamira ya kukidhi moja ya vigezo vya kuwa jiji lakini pia kuwaletea wananchi maendeleo. Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amesema anasikitika sana kuona Halmashauri ya manispaa ya Morogoro inakuwa na mazingira machafu muda wote, likiwemo soka la Mawenzi. hivyo, amewataka watendaji kufanya jitihada na kutafuta mbinu mbadala za kutatua changamoto hiyo ya kuusafisha mji huo ili kuhakikisha mazingira ya manispaa hiyo yanakuwa safi. Sanjari na hilo Dkt. Mussa amewataka watendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanakusanya kodi kwa wafanyabiashara wote wa mji huo, kwani kuna kila dalili za manispaa hiyo kutokusanya kodi kwa baadhi ya wafanyabiashara au kama kodi hiyo inakusanywa basi haiingizwi kwenye mifuko ya Serikali. Naye Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Rebeca Nsemwa amesema Halmashauri hiyo ina mpango wa kuupanga mji huo kuwa wa kisasa zaidi ikiwa ni pamoja na kuondoa vibanda ambavyo vimekaa maeneo yasiyo sahihi, kupanga biashara mahali panapo stahili na kutoza faini kwa wale watakaobainika kuchafua mazingira ya manispaa hiyo ili kuhakikisha usafi unazingatiwa hususan kipindi hiki cha kujipanga kuelekea Morogoro kuitwa Jiji. MWISHO.

RC MALIMA AWAWASHIA MOTO KWA MKURUGENZI NA AFISA MIPANGO MIJI MANISPAA MOROGORO
▶︎

RC MALIMA AWAWASHIA MOTO KWA MKURUGENZI NA AFISA MIPANGO MIJI MANISPAA MOROGORO

RC TABORA AAGIZA KUKAMATWA KWA WATUMISHI 3 NA MMILIKI WA ZAHANATI YA HOSSIANA KWA KULAZA WAGONJWA
▶︎

RC TABORA AAGIZA KUKAMATWA KWA WATUMISHI 3 NA MMILIKI WA ZAHANATI YA HOSSIANA KWA KULAZA WAGONJWA

🔴#LIVE Kutoka MOROGORO: GOOD MORNING NA RC ADAM MALIMA | 10 JULY 2023
▶︎

🔴#LIVE Kutoka MOROGORO: GOOD MORNING NA RC ADAM MALIMA | 10 JULY 2023

RC Malima awataka madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kupunguza hoja za CAG
▶︎

RC Malima awataka madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kupunguza hoja za CAG

🔴#Live: RAIS SAMIA - "MOROGORO KUWA JIJI BADO SANA -TUTAWALIPA HISANI MLIYOTUPA" -MKUTANO wa HADHARA
▶︎

🔴#Live: RAIS SAMIA - "MOROGORO KUWA JIJI BADO SANA -TUTAWALIPA HISANI MLIYOTUPA" -MKUTANO wa HADHARA

MWANAFUNZI AJIFUNGUA CHOONI TABORA-RC CHACHA ACHARUKA
▶︎

MWANAFUNZI AJIFUNGUA CHOONI TABORA-RC CHACHA ACHARUKA

#RC MANYARA AMFUTA KAZI MWALIMU KWA UBADHIRIFU
▶︎

#RC MANYARA AMFUTA KAZI MWALIMU KWA UBADHIRIFU

England vs. DR Congo Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau
▶︎

England vs. DR Congo Highlights FIFA World Cup 2026 | Sportschau

DAWA YA RUTO!! Listen to what new DCP SG Methu said today in Olkalou after goons attacked them
▶︎

DAWA YA RUTO!! Listen to what new DCP SG Methu said today in Olkalou after goons attacked them

#KũmuramuraMagathĩti 02\07\26
▶︎

#KũmuramuraMagathĩti 02\07\26

MAPYA YAIBUKA 'MAFURIKO KUIKIMBIA' CHADEMA
▶︎

MAPYA YAIBUKA 'MAFURIKO KUIKIMBIA' CHADEMA

WADAU WA BARABARA MOROGORO WAWEKA MIKAKATI YA MATENGENEZO YA BARABARA.
▶︎

WADAU WA BARABARA MOROGORO WAWEKA MIKAKATI YA MATENGENEZO YA BARABARA.

RC MALIMA AKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOA WA TANGA, ASISITIZA MSHIKAMANO WA KITAIFA.
▶︎

RC MALIMA AKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOA WA TANGA, ASISITIZA MSHIKAMANO WA KITAIFA.

MIKAKATI YA MKOA WA MOROGORO YAWEKWA WAZI MBELE MBIO ZA MWENGE WA UHURU.
▶︎

MIKAKATI YA MKOA WA MOROGORO YAWEKWA WAZI MBELE MBIO ZA MWENGE WA UHURU.

MIRADI YA SHS. BILIONI 2.8 KUTEMBELEWA NA MWENGE MKINGA, DC KALIMA AWAITA WANANCHI
▶︎

MIRADI YA SHS. BILIONI 2.8 KUTEMBELEWA NA MWENGE MKINGA, DC KALIMA AWAITA WANANCHI

Viongozi vyama vya ushirika wahimizwa kuzingatia weledi.
▶︎

Viongozi vyama vya ushirika wahimizwa kuzingatia weledi.

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.
▶︎

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.

INASIKITISHA BAADHI YA MASHABIKI WA MNYAMA WAFURAHIA PACOME KUUMUA | HAWAJAENDA KUMUONA HOSPITALI
▶︎

INASIKITISHA BAADHI YA MASHABIKI WA MNYAMA WAFURAHIA PACOME KUUMUA | HAWAJAENDA KUMUONA HOSPITALI

NYIMBO ZA KUABUDU | DEEPEST SWAHILI WORSHIP & PRAYER SONGS
▶︎

NYIMBO ZA KUABUDU | DEEPEST SWAHILI WORSHIP & PRAYER SONGS

KAKONKO YAKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO KWA WAKATI
▶︎

KAKONKO YAKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO KWA WAKATI