RC Malima awataka madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kupunguza hoja za CAG

RC Malima awataka madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kupunguza hoja za CAG Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi wametakiwa kuwasimamia watendaji wa halmashauri yao ili  kuepusha hoja za ukaguzi kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Agizo hilo limetolewa Julai 1, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, wakati wa kikao cha kupitia na kukagua hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika Wilayani. Mhe. Malima amesema, katika mwaka wa fedha 2025/2026, halmashauri hiyo ya Malinyi imepata jumla ya hoja 33 za ukaguzi, ambapo nyingi zimesababishwa na uzembe wa baadhi ya watendaji kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa weledi, hali iliyochangia kujitokeza kwa dosari katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. "..Hapa pana elementi ya uzembe. Kama kuna elementi ya ubadhirifu, tunawasubiri TAKUKURU..." amesema Mhe. Adam Malima. Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa amepongeza uongozi wa Halmashauri ya hiyo kwa usimamizi na utendaji kazi mzuri, jambo lililochangia kutekeleza vema maendeleo ya wananchi wa Malinyi, Mkoa wa Morogoro na Taifa kwa ujumla. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Ngohelanga Jenas Jonas Kyerike  amesema sheria na taratibu ziko wazi kuwa hakuna ujenzi wowote unaopashwa kuendelea bila kupata vibali kutoka kwa wataalamu husika. Ameongeza kuwa ni muhimu kuwepo kwa uwajibikaji kwa viongozi wanaohusika na ufujaji wa mali za umma kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa, amewataka watumishi wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanayafahamu na kuyasimamia ipasavyo mambo yote yanayotekelezwa katika halmashauri. Pia amewasisitiza kujiepusha na migogoro inayoweza kuathiri utendaji kazi, pamoja na kuacha tabia ya kuomba uhamisho mara kwa mara. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, ameongoza vikao vya kupitia na kukagua hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri za Wilaya za Malinyi na Ulanga Leo, Julai 2, 2026, ataendelea na vikao hivyo katika Halmashauri ya Mlimba na Halmashauri ya Mji wa Ifakara. Mwisho.

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST
▶︎

MBUNGE MUSUKUMA AKIELEZA MAGUMU ALIYOPITIA KATIKA SIASA NA BIASHARA | M&S PODCAST

Dr Joe Njagi 🎙️ | “You Can Do It If You Want To” — Dr Manu Chandaria
▶︎

Dr Joe Njagi 🎙️ | “You Can Do It If You Want To” — Dr Manu Chandaria

DEREVA WA HECHE AFARIKI NYUMBA YA KULALA WAGENI KIGOMA, MWILI WAKUTWA CHINI
▶︎

DEREVA WA HECHE AFARIKI NYUMBA YA KULALA WAGENI KIGOMA, MWILI WAKUTWA CHINI

🔴DIRECT Assemblée NATIONALE: Le PM Ousmane Sonko face aux députés
▶︎

🔴DIRECT Assemblée NATIONALE: Le PM Ousmane Sonko face aux députés

How Nyawira Muraguri Built Wealth Before Age 35
▶︎

How Nyawira Muraguri Built Wealth Before Age 35

DEEP SWAHILI WORSHIP 2026 🔥 Ombi Langu | Hakuna Mungu Kama Wewe | Best Nonstop Prayer & Gospel Mix
▶︎

DEEP SWAHILI WORSHIP 2026 🔥 Ombi Langu | Hakuna Mungu Kama Wewe | Best Nonstop Prayer & Gospel Mix

ACT REMOVES THE MASKS AND MOVES THE WAY FORWARD TO SAY THE UNSAYED
▶︎

ACT REMOVES THE MASKS AND MOVES THE WAY FORWARD TO SAY THE UNSAYED

RC MALIMA AKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOA WA TANGA, ASISITIZA MSHIKAMANO WA KITAIFA.
▶︎

RC MALIMA AKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOA WA TANGA, ASISITIZA MSHIKAMANO WA KITAIFA.

Wewe ni Sababu / Mataifa Yote / Yale Umetenda // Deep Swahili Worship mix
▶︎

Wewe ni Sababu / Mataifa Yote / Yale Umetenda // Deep Swahili Worship mix

How I became Super Rich Without Ever being Employed!!MP Ndindi Nyoro!!
▶︎

How I became Super Rich Without Ever being Employed!!MP Ndindi Nyoro!!

Viongozi vyama vya ushirika wahimizwa kuzingatia weledi.
▶︎

Viongozi vyama vya ushirika wahimizwa kuzingatia weledi.

China Has Launched New Generation Transport SHOCKING The US
▶︎

China Has Launched New Generation Transport SHOCKING The US

Hello! #ThePeoplesBreakfast Is LIVE! We Look at Kenya's Sign Language Bill & Ethnic Rhetorics
▶︎

Hello! #ThePeoplesBreakfast Is LIVE! We Look at Kenya's Sign Language Bill & Ethnic Rhetorics

Jimi Wanjigi: There is 2 trillion that we do not know where it is coming from. We are living a lie
▶︎

Jimi Wanjigi: There is 2 trillion that we do not know where it is coming from. We are living a lie

WADAU WA BARABARA MOROGORO WAWEKA MIKAKATI YA MATENGENEZO YA BARABARA.
▶︎

WADAU WA BARABARA MOROGORO WAWEKA MIKAKATI YA MATENGENEZO YA BARABARA.

RHUMBA  MIX 2022 BEST OF RHUMBA SONGS MIX 2022 RHUMBA DRIVE  MIX 2022   DJ LANCE THE MAN  /RH EXCLU
▶︎

RHUMBA MIX 2022 BEST OF RHUMBA SONGS MIX 2022 RHUMBA DRIVE MIX 2022 DJ LANCE THE MAN /RH EXCLU

TENZI ZA ROHONI - DEEP RELAX SWAHILI WORSHIP SONGS
▶︎

TENZI ZA ROHONI - DEEP RELAX SWAHILI WORSHIP SONGS

UKITAKA NDOA YENYE FURAHA, SIRI NI MOJA TU
▶︎

UKITAKA NDOA YENYE FURAHA, SIRI NI MOJA TU

RHUMBA MIX VJ JONNIE 254  | OLIVER N'GOMA, MADILU SYSTEM, PAPA WEMBA, MBILIA BEL, KANDA BONGO MAN
▶︎

RHUMBA MIX VJ JONNIE 254 | OLIVER N'GOMA, MADILU SYSTEM, PAPA WEMBA, MBILIA BEL, KANDA BONGO MAN

SHEIKH MWAIPOPO AMPASUA VIBAYA SANA USTADH JUMA NA MUSOMA "UMEINGIA CHOO CHA KIKE"
▶︎

SHEIKH MWAIPOPO AMPASUA VIBAYA SANA USTADH JUMA NA MUSOMA "UMEINGIA CHOO CHA KIKE"