WAZIRI ULEGA ATOA SAA 72 MAWASILIANO DARAJA LA GONJA MPIRANI YAREJEE
Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega ametoa saa 72 kwa Wakala ya Barabara nchini (TANROADS) mkoa wa Kilimanjaro kurejesha mawasiliano katika daraja la Gonja Mpirani. Hatua hiyo inafuatia kuvunjika kwa daraja hilo hivi karibuni kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha katika safu ya milima ya Pare Wilayani Same. " Ndugu zangu poleni sana kwa changamoto iliyotokea, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amenituma niwape pole na niwahakikishie ujenzi wa daraja jipya utakamilika ndani ya siku tatu ili muendelee na shughuli zenu kama kawaida", amesema Ulega. Amemtaka Mtendaji mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta kuhakikisha wataalam kutoka makao makuu wanashirikiana na wa mkoa kufanya kazi usiku na mchana ili mawasiliano ya Ndungu-Maore yarejee. " Kipimo cha ufanyakazi mzuri wa meneja wa TANROADS itakuwa ni uwezo wake kukabiliana na dharura na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati", amesisitiza Ulega. Amezungumzia umuhimu wa mameneja wote wa TANROADS nchini kuchukua tahadhari kuelekea msimu wa mvua za masika ili kuepuka magari kukwama na usumbufu kwa wasafiri. Naye Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu ameipongeza TANROADS kwa kuchukua hatua za haraka katika kurudisha mawasiliano katika barabara hiyo. Daraja la Gonja Mpirani liko katika barabara ya Same-Mkomazi Km 105 na linaunganisha kata za Ndungu na Maore.

WAZIRI ULEGA AWATAKA WAKANDARASI DODOMA RING ROAD KUONGEZA KASI

WIZARA YA UJENZI YAANIKA MIKAKATI KUIKIJANISHA DODOMA KUELEKEA DIRA 2050

The Gallery of Ruto's Lies PART 1: Kenyans furious as Ruto’s promises turn into empty projects

DKT. MWIGULU AAGIZA SULUHU YA KUDUMU DARAJA LA MAGOLE –DUMILA

Man Cave 6: Pressure, Power and Purpose

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UJENZI WA BARABARA YA NJIA SITA DODOMA–CHAMWINO IKULU

Albin Kurti ia plaste në sy mes Kuvendit Edi Ramës: Ja si bëhet atdheu

TANROADS: ULINZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA MADARAJA NI JUKUMU LA KILA MWANANCHI

Runda's hidden gem revealed - 37 by Ineza | Property Focus with PJ Ngigi

Fahamu Kuhusu Mamlaka ya Usafiri Wa Anga Tanzania (TCAA)

SHUHUDIA ULIPOFIKA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE SHINYANGA, RC MHITA ATEMBELEA UJENZI WAKE, NDEGE KUBWA.

MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI, WAZAWA WANUFAIKE NA AJIRA ZILIZOPO.

MRADI WA UMEME WA JUA KISHAPU KUZALISHA MEGAWATI 150

WAZIRI ATOA SIKU 28 KUVUNJA MKATABA NA MKANDARASI, ATOA MAAGIZO MAZITO

Michelle Obama speech brings tears to Barack | Watch it in full

NEW AIRPORT INSIDE THE NYERERE NATIONAL PARK

Has the Iran war changed fuel forever? | ABC News Daily podcast

VIJANA WAJENGEWA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU

Kush eshte Dritan Goxhaj? Flet Ilir Kulla | Zone e Lirë

