LOWASSA ATANGAZA KURUDI CCM, 'NIMERUDI NYUMBANI'

Waziri Mkuu wa zamani, #Edward #Lowassa Ijumaa Machi Mosi, 2019 ametangaza uamuzi wa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM). Lowassa amerejea katika chama chake cha zamani shughuli iliyofanyika ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni Rais wa Tanzania, John #Magufuli.