Omollo atupilia mbali madai ya utekaji, KNCHR yaibua maswali

Katibu wa usalama Raymond Omollo sasa anasema visa vya watu wanaodai kutekwa nyara ni vya kupangwa. Omollo akiitetea serikali dhidi ya madai yoyote ya kuhusika na visa vya utekaji nyara vinavyoripotiwa. Haya yanajiri huku tume ya kitaifa ya kutetea haki ya KNCHR ikiilaumu serikali kwa namna ilivyoshughulikia maandamano ya wiki jana ambapo inasema watu saba walitekwa nyara.