Hofu yatanda Bonde la Kerio kutokana na wizi wa mifugo

Hofu imetanda katika baadhi ya sehemu za Bonde la Kerio kufuatia kurejea kwa visa vya wizi wa mifugo, huku familia kadhaa zikihama makao yao. Wakazi waliosalia wanaishi kwa hofu baada ya zaidi ya mifugo mia mbili kuibwa katika muda wa wiki mbili zilizopita. Hali hii tete imeripotiwa licha ya maafisa wa usalama kuendesha operesheni ya kutwaa silaha haramu.