PART TWO: MUNGU ALITUMIA MIAKA 7,000 KUKAMILISHA UUMBAJI
#Uumbaji#HapoMwanzo#Mungu#Genesis Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia. Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji. Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza. Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.” Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili. Mungu akasema, “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, nchi kavu itokee.” Ikawa hivyo. Mungu akapaita mahali pakavu “Nchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema. Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu. Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka, na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia, ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne. Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.” Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema. Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni, muongezeke, muyajaze maji ya bahari; nao ndege waongezeke katika nchi.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tano. Mungu akasema, “Nchi na itoe aina zote za viumbe hai, wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo na wanyama wa porini wa kila aina.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.

What Is The Blood Covenant? The Key To Understanding The Bible - Dr. Myles Munroe | MunroeGlobal.com

MUST WATCH 😱 The Forgotten Language Of Creation | Prophet Uebert Angel

MELCHIZEDEK niwe muntu wamayobera muri bibiliya,niwe mayobera yambere atarasobanuka muri bibiliya

The Book of Enoch Explained: What Happens After Death?

MITIMINGI # 244 UNAPOTAKA KUOA/KUOLEWA ANGALIA MTU ATAKAEKUVUTIA WEWE KIROHO NA KIMWILI

ISRAELI NA UKWELI USIOJULIKANA // AHADI INAYOTIMIA SASA

MAISHA YAKO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO // SPIRITUAL REALM

DUNIA NZIMA YAANGAMIA,WATU 8 WAPONA KATIKA SAFINA YA NUHU

All 7 Dimensions Explained in Detail (From 0D to Infinity)

LILITH- MWANAMKE ALIYEGEUKA NYOKA EDENI NA KUMDANGANYA EVA

Professor Jiang: World War 3 Is About To Begin, Let Me Explain!

Ancient Structures That Look Like Future Architecture

ISRAEL KATIKA UNABII - WAYAHUDI WALIOPO ISRAEL NDIO WALEWALE WALIOPO KWENYE BIBLIA?

UKWELI KUHUSU NYOKA KWENYE BUSTANI YA EDENI.

ታቦተ ጽዮንን ፍለጋ - መባዕ ቲቪ (Meba TV) @Meba_tv

UKWELI WA BIBLIA KUHUSU KIFO

7 Ancient Discoveries That Defy All Explanation

Fall Asleep to the Gospel of Mark | Mark 1-16

ELIZABETH MOKORO AMUA KUSEMA UKWELI NOMINAL SDA NA KUWAAMBIA WATOKE GC ISHAPOTOKA

