UKWELI KUHUSU NYOKA KWENYE BUSTANI YA EDENI.
#SIRIZABIBLIA#MWANZO#UUMBAJI#BIBLIA#MUNGU Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia. Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji. Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza. Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.” Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili. Mungu akasema, “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, nchi kavu itokee.” Ikawa hivyo. Mungu akapaita mahali pakavu “Nchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema. Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu. Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka, na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia, ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne. Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.” Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema. Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni, muongezeke, muyajaze maji ya bahari; nao ndege waongezeke katika nchi.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tano. 24Mungu akasema, “Nchi na itoe aina zote za viumbe hai, wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo na wanyama wa porini wa kila aina.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema. Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.”

#Mkasa wa Dereva Lori aliyemkanyaga Nyoka Mlima Kitonga /Akumbwa na tabu na Mateso.

KISA CHA KICHOCHORO CHA KWENDA PEPONI (Simulizi Ya Mnara Wa Babeli)

Maombı yana Nguvu ya Uumbajı

Utukufu Juu Ya Maisha Yako

Jinsi Ya Kua Na Uwepo Wa Mungu

Possessing Your Possessions I

HOW TO WAIT ON THE LORD IN PRAYER

The Price Of Being In God

ISRAELI NA UKWELI USIOJULIKANA // AHADI INAYOTIMIA SASA

BABELI:MJI WA KWANZA KUJENGWA BAADA YA GHARIKA/NIMRODI

The story book : UKWELI WOTE KUHUSU BUNDI NA FAIDA ZAKE

TAFSIRI YA NDOTO UNAPOMUONA NYOKA USINGIZINI

30 Real Life Superheroes | Random Acts of Kindness That Will Make You Cry #8

MWISHO WA DUNIA UNA MAMBO MAZITO YA KUTISHA...!!

KABLA YA KUOMBA,FAHAMU KWANZA MUNGU ALIPO

LILITH- MWANAMKE ALIYEGEUKA NYOKA EDENI NA KUMDANGANYA EVA

7. DALILI ZA KURUDI KWA YESU NA UNYAKUO WA KANISA | Mwl. Isaac Javan

What the First Word of Genesis Actually Says in Hebrew

the story book Jamal April. liko wapi sanduku la agano?

