Linda Mwananchi wapendekeza Sifuna kupeperusha bendera ya upinzani 2027

Viongozi wa mrengo wa Linda Mwananchi wamevitaka vyama vya upinzani kumuunga mkono Seneta wa Nairobi, Edwin Sifuna, kama mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Wakizungumza mjini Bungoma, viongozi hao walisema eneo la Magharibi liko tayari kumpa Sifuna uungwaji mkono wa hali na mali ili kuhakikisha anaingia Ikulu. Aidha, wameiitaka Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuhakikisha uchaguzi wa mwaka 2027 unakuwa huru, wa haki na wenye kuaminika. Viongozi hao pia wamesisitiza kuwa watasimama kidete kulinda kura zao ili kuhakikisha matokeo ya uchaguzi yanaakisi matakwa ya wananchi. Melita Oletenges ana taarifa zaidi.