RC Kunenge Awataka Wafugaji Kisarawe Kufuga Kisasa Kuinua Uchumi na Kukidhi Soko la Kimataifa
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amewataka wafugaji wa Wilaya ya Kisarawe kufuga kisasa ili kuongeza mnyororo wa thamani wa nyama na kuinua uchumi wao pamoja na kuhimili ushindani wa soko la kimataifa. Mhe. Kunenge ametoa rai hiyo leo wakati wa kikao chake na wafugaji wa Wilaya ya Kisarawe kilichofanyika katika Kata ya Mzenga. Akizungumza katika kikao hicho, amesema kuwa kutokana na ushindani wa soko la nyama duniani, ni muhimu kwa wafugaji kuhakikisha mifugo na bidhaa zake zinazingatia viwango na vigezo vinavyotakiwa kimataifa. Aidha, amesisitiza matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro kati ya wakulima na wafugaji. “Ardhi haiongezeki bali watu wanaongezeka, hivyo ni lazima tufuge kwa tija. Tunapaswa kutenga maeneo maalum ya ranchi ndogo ili kuepuka ufugaji holela unaosababisha migogoro,” amesema Mhe. Kunenge. Ameeleza kuwa Mkoa wa Pwani una jumla ya ranchi ndogo 847, huku akisisitiza umuhimu wa wafugaji kumilikishwa maeneo rasmi kwa ajili ya ufugaji huo. Aidha, amesema idadi ya mifugo inayofugwa inapaswa kuendana na ukubwa wa eneo lililotengwa ili kuongeza tija na kuzuia uharibifu wa mazingira. Mhe. Kunenge amesema dhamira ya Serikali ni kuifanya sekta ya ufugaji kuwa ya kisasa na yenye tija kwa kuondoa migogoro kati ya wakulima na wafugaji pamoja na kuongeza kipato cha wafugaji. Sambamba na hilo, amekemea baadhi ya wafugaji waliopatiwa hati za umiliki wa ranchi ndogo kwa kuuza maeneo hayo kinyume cha utaratibu, na kuwataka warejeshe maeneo hayo Serikalini. Kwa upande wao, baadhi ya wafugaji wamemuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kuchimbiwa mabwawa ya maji na kujengewa majosho kwa ajili ya mifugo yao, wakieleza kuwa kwa sasa wanalazimika kusafirisha mifugo umbali mrefu kutafuta maji. Vilevile, wameomba kupatiwa wataalamu wa kuwapa elimu ya ufugaji bora wenye tija ili waweze kuongeza uzalishaji na kipato chao.

MANISPAA YA KIBAHA YATOA TSH MILIONI 991.5 KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU...

NILIMUOMBA KAKA ANILIPIE KODI YA MIEZI MITATU NIBAKI DAR | NIMETOKA KIJIJINI SANA | MAJID NSEKELA

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

CORECU yatakiwa kuhakikisha wakulima wanazingatia uzalishaji wenye tija ili kukuza uchumi wao na kuo

Pakistani Truck Parts Repair with a Master Mechanic Amazing Restoration

Rc Kunenge, amewapongeza wafanyakazi kwa bidii na weledi wao uliosaidia mkoa huo kuongoza katika mae

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

Is Kenya Ready to Invest in Its Science Future?

RC KUNENGE AONGOZA KIKAO KAZI NA WATENDAJI KATA ZOTE PWANI...

When Tyson Faced the Smash Machine

HISTORIC COMEBACK BY THE GREATEST JAPANESE GENERATION OF ALL TIME AGAINST ANCELOTTI’S BRAZIL

How Traore is Magically Growing Real Apples in Desert?

This is the way ugandans can do to get capital and stop going to middle East for work

Inside the Largest Wood Sawmill Factory – How Plywood Is Made From Logs to Table (Full Process)

FULL VIDEO KILICHOMPONZA MWENYEKITI WA MTAA HADI RC CHALAMILA KUAGIZA AKAMATWE | UTAPELI WA VIWANJA.

BREAKING: Pwani Kuzalisha Mboga na Matunda Kulisha Dar na Zanzibar – Waziri Chongolo Afunguka...

START YOUR TUESDAY WITH FAITH | TODAY GOD IS GIVING YOU UNEXPECTED OPPORTUNITIES | FATHER FREDDY ...

RC KUNENGE AZINDUA KIWANDA KIKUBWA CHA MAGODORO AFRIKA MASHARIKI

From Nothing to a Wealthy Chicken Farmer on the Smallest Space

