BREAKING: Pwani Kuzalisha Mboga na Matunda Kulisha Dar na Zanzibar – Waziri Chongolo Afunguka...
#HabariZaLeo #TanzaniaNews #KilimoTanzaniaKibaha, Pwani – Machi 16, 2026 Serikali imeanza mkakati wa kuufanya Mkoa wa Pwani kuwa kitovu cha uzalishaji wa mboga mboga na matunda yatakayolisha masoko ya Dar es Salaam na Zanzibar. Hatua hiyo inalenga kuongeza uzalishaji wa mazao, kuimarisha usalama wa chakula na kufungua fursa zaidi za ajira kwa vijana na wakulima. Akizungumza Machi 16, 2026 mjini Kibaha, Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo amesema Mkoa wa Pwani umechaguliwa kuwa mfano katika uzalishaji wa mboga mboga na matunda kwa kuzingatia ubora, viwango na tija ya kilimo. Amesema mradi huo kwa awamu ya kwanza utaanza katika eneo la hekari 200 huku serikali ikiendelea kukamilisha taratibu na maandalizi ya utekelezaji wake. Aidha, amesema mpango huo ni sehemu ya kutekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha uzalishaji wa chakula na kuhakikisha Tanzania inachangia kulisha Afrika na dunia. Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema mpango huo pia unalenga kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuongeza ajira kwa vijana kupitia sekta ya kilimo. Ameeleza kuwa Wilaya ya Kibaha ina zaidi ya hekari 1,000 zinazofaa kwa kilimo hicho ambapo kwa kuanzia zitatumika hekari 200, huku Wilaya ya Kisarawe ikiwa na takribani hekari 1,500 zitakazotumika kwa kilimo cha umwagiliaji mwaka mzima kwa kuzingatia utaalamu wa kisasa wa kilimo. Usisahau: 👍 Like 💬 Comment 🔔 Subscribe kupata habari na taarifa muhimu kila siku.

KUNENGE AHAMASISHA UWEKEZAJI MKANGE

DC ATOA SIKU 14 ZA UCHUNGUZI SAKATA LA MABAUNSA WANAODAIWA KUVUNJA MAGETI YA MAKAZI UPANGA

Rc Kunenge, amewapongeza wafanyakazi kwa bidii na weledi wao uliosaidia mkoa huo kuongoza katika mae

MANISPAA YA KIBAHA YATOA TSH MILIONI 991.5 KWA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU...

RC Kunenge Awataka Wafugaji Kisarawe Kufuga Kisasa Kuinua Uchumi na Kukidhi Soko la Kimataifa

Mkoa wa Pwani wajipanga utekelezaji wa Dira 2030 katika uwekezaji

MAAFISA UGANI WAPATIWA MAFUNZO KUIMARISHA UZALISHAJI WA KOROSHO

RC KUNENGE AONGOZA KIKAO KAZI NA WATENDAJI KATA ZOTE PWANI...

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

PARLIAMENTARY COMMITTEE CONGRATULATES DART

RC Kunenge, amelitaka Jeshi la polisi Mkoa wa Pwani kuzingatia utii, nidhamu na weledi kazini

Traoré’s Massive Irrigation Network Is Stunning the World

RC KUNENGE AZINDUA KIWANDA KIKUBWA CHA MAGODORO AFRIKA MASHARIKI

WAZIRI ULEGA AOMBA MKURANGA KUWA MANISPAA

Ndoa 130 Zafungwa Siku Moja Dar! Waziri Katambi Atoa Ujumbe Mzito...

MWANAMKE ALIYE MTEKA MTOTO SHULENI NA KUTAKA ALIPWE MILIONI 20,AKAMATWA NA MTOTO TABORA

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

WATU KUTOKA KINSHASA WA WASILI KAZIMIA KUTAZAMA MRADI WAO

tagesschau 20:00 Uhr, 13.06.2026

