KASEKENYA ATOA MIEZI SABA KUKAMILIKA UJENZI WA OSBP MANYOVU

Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya amemtaka mkandarasi China Jiangxi International Economic and Technical Cooperation Co. Ltd anaejenga kituo cha forodha cha pamoja (OSBP) Manyovu/Mugina kuhakikisha kinakamilika ifikapo Julai mwaka huu. Kituo hicho cha mfano cha forodha kinachojegwa Manyovu wilayani Buhigwe mkoani Kigoma katika mpaka wa Tanzania na Burundi kinatarajiwa kuwaweka wadau wote wa huduma za mpakani na fedha katika eneo moja na hivyo kuchochea ukuaji wa biashara kati ya Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.