MICHE LAKI 5 YA KAHAWA YAGAWIWA BURE KWA WAKULIMA MKOANI KILIMANJARO.
Serikali kupitia Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) imeendelea kuonesha dhamira yake ya dhati katika kuimarisha sekta ya kahawa na kuinua uchumi wa wakulima kwa kuzindua zoezi la ugawaji wa miche zaidi ya laki tano ya kahawa bure kwa wakulima wa Mkoa wa Kilimanjaro. Akizungumza katika uzinduzi wa zoezi hilo lililofanyika tarehe 30 Machi 2026 katika Kijiji cha Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Jimbo la Vunjo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mheshimiwa Nurdin Hassan Babu, aliipongeza Serikali kwa jitihada zake za kuendeleza zao la kahawa, akieleza kuwa ni uti wa mgongo wa uchumi wa Mkoa huo. Aidha, aliwataka wakulima kuacha mara moja tabia ya kukata miti ya kahawa na badala yake kuendeleza mashamba yao ili kuongeza uzalishaji. Mheshimiwa Babu pia aliwahimiza vijana kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali kupitia sekta ya kilimo cha kahawa, akisisitiza kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi na kuhakikisha zao hilo linaendelea kuwa nembo ya Mkoa wa Kilimanjaro. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania, Bw. Primus Kimaryo, alieleza kuwa ugawaji wa miche hiyo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuongeza uzalishaji wa kahawa nchini na kuboresha kipato cha wakulima. Aliwataka wakulima kuhakikisha wanapanda miche wanayoipokea ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa, huku akisisitiza kuwa hatua hiyo ni ya kihistoria katika kuwawezesha wakulima na kukuza zao hilo la kimkakati. Zoezi hili linatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo kwa wakulima wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa kuongeza uzalishaji, kuinua kipato cha wananchi, na kufungua ajira zaidi hususan kwa vijana. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha sekta ya kahawa inazidi kukua na kuwa na tija kwa taifa.

Tazama furusa Kwenye kilimo Cha zao la Nanasi ( Video)

BODI YA KAHAWA KUGAWA MICHE MILIONI 20 YA RUZUKU BURE KWA WAKULIMA NCHINI.

Kisumu: Mwanamke mmoja abadilisha urithi kuwa uhuru kwa kukumbatia ufugaji wa nyuki

GUMZO!! MBUNGE HUYU MZANZIBARI ATOA ONYO LA KUUWAWA KWA WANAOZUNGUMZIA MUUNGANO NA KUZUA TAHARUKI

ZABIBU INAWEZA KULIMWA NCHI NZIMA|DODOMA ZABIBU HUVUNWA MARA MBILI KWA MWAKA

TANZANIA COFFEE AUCTION 15 JANUARY 2026

WAGANGA WA TIBA ASILI NA TIBA MBADALA WASOGEZEWA HUDUMA YA USAJILI JIRANI BARIADI DC

KINSHASA HADI KAZIMIA MASHAMBANI - MKUU WA SHIRIKA AFUNGUKA

👉 “Inside a 3,000 Acre Mango Farm in Africa Graduate Farmer’s Success Story”

How I Was Deported From The US

Hybrid vs Dwarf vs Tall Coconut: Why Hybrid Coconut is the Most Profitable Choice

IMARA F1 MBEGU PEKEE INAYOWEZA KUVUMILIA WADUDU WA KANTANGAZE

AgroLink - Coconut Farming in Ghana

TCB YATEKELEZA MAMBO HAYA MUHIMU KUELEKEA MWAKA MPYA WA FEDHA 2026/27

FISH FARMING IN UGANDA POND PREPARATION

NJIA BORA ZA KUVUNA, HULINDA UBORA NA THAMANI YA KAHAWA

KILIMO CHA UFUGAJI SAMAKI (KINYESI CHA NG'OMBE PIA NI CHAKULA KWA SAMAKI)

KILIMO AJIRA YANGU-TARI KUWEZESHA KILIMO CHA KARANGA MIKOA YA DODOMA,SINGIDA NA GEITA

WAJUMBE WA BODI ZA USULUHISHI WA NDOA WILAYANI KYERWA DC WAJENDEWA UWEZO

