Hatua Kubwa Ufugaji Zanzibar! Kikundi cha Bambi Chapewa Ardhi ya Malisho
Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Mhe. Suleiman Masoud Makame, ameagiza kutolewa hekari tano kwa kikundi cha Wafugaji wa Maendeleo Kwanza cha Bambi, kwa ajili ya kuimarisha uzalishaji wa chakula cha mifugo. Agizo hilo amelitoa akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Kusini, Wilaya ya Kati, alipokutana na wafugaji wa Bambi wanaonufaika na mradi shirikishi wa wasindikaji na wazalishaji wa maziwa Tanzania — Ti3P, ambapo tayari wamepatiwa ng’ombe 19. Aidha, Waziri Suleiman Masoud Makame ameielekeza Idara ya Maendeleo ya Mifugo kuchagua watu wawili kutoka katika kikundi hicho ambao watakwenda mkoani Arusha kujifunza mbinu bora za ufugaji kwa mfugaji aliyepiga hatua, ili kuongeza ujuzi na ushirikiano baina ya wafugaji. Kwa upande wake, Kiongozi wa Wafugaji wa Maendeleo Kwanza, Bwana Hamid Abdallah, ameishukuru Serikali kwa kuwapatia eneo la malisho na kwa kuwashirikisha wafugaji katika kila hatua ya utekelezaji. Ameahidi kuendeleza jitihada za kuongeza uzalishaji wa maziwa kupitia ng’ombe waliopatiwa. Mradi huu wa Ti3P umeendelea kuwanufaisha wafugaji Zanzibar, ambapo hadi sasa jumla ya ng’ombe 246 zimetolewa — ng’ombe 93 Unguja na ng’ombe 153 Pemba katika lengo la kuongeza upatikanaji wa maziwa kwa uhakika nchini.

KIPINDI: MWONGOZO WA MALISHO

Ruto heart attack as Sifuna and his troop holds Mega Rally in Thika with 'Sisi Ndio Sifuna!'

Kamati ya Uongozi ya Mradi wa TFSRP Yakagua Maendeleo ya Miradi Zanzibar

DAWA YA RUTO!! Listen to Gachagua Powerful remarks today in Bungoma Church destroying Kasongo badly!

TASAF KILOSA YAZISAJILI KAYA ZENYE VIASHIRIA VYA KUKUMBWA NA MAFURIKO

Kilimo Almasi | Ufugaji wa ng'ombe wa maziwa

UFUGAJI WA NG'OMBE UNAVYOWANUFAISHA VIJANA

Mzee Mkulima na Siri ya Kubadili Kilimo kuwa Biashara ya Utalii

#KILIMOBORA: UFUGAJI WA NG'OMBE WA MAZIWA - 17082024

A-Z BIASHARA YA MIFUGO TANZANIA /MASOKO , MNYORORO WA THAMANI,VIBALI NA LESENI

MRADI WA MAZIWA FAIDA UNAOTEKELEZWA NA TALIRI ULIVYOMNUFAISHA MFUGAJI

From 1 cow to 150 cows in 3 years: The power of good management

Naglabasan Ang GT ! inabot Ng Dilim Kakahila Ng isda

TALIRI OPEN DAY 2026

JIFUNZE_NJIA_BORA_ZA_UFUGAJI_WA_NGOMBE_WA_MAZIWA_KITAALAMU_ZAIDI_

#HIGHLIGHTS TCCS COMMERCIAL LIVESTOCKSHOW & AUCTION | UBENA ZOMOZI

NBC Tanzania | NBC na Mbogo Ranches Wasaidia Wafugaji Kufikia Malengo

ZAIDI YA WAFUGAJI 3,000 MUHEZA WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UFUGAJI BORA KUPITIA MRADI WA MAZIWA FAIDA

Bwana Namli anauza maziwa ya mbuzi Zanzibar kwa bei ya Shilingi 7,000 kwa lita moja

