ZAIDI YA WAFUGAJI 3,000 MUHEZA WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UFUGAJI BORA KUPITIA MRADI WA MAZIWA FAIDA

Zaidi ya wafugaji 3,000 kutoka wilaya ya Muheza mkoani Tanga Region wamepata fursa ya kunufaika na mafunzo ya ufugaji bora wa kisasa kupitia Mradi wa Maziwa Faida unaotekelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti, Ushauri na Mafunzo ya Kilimo na Chakula nchini Ireland (Teagasc) kwa ufadhili wa Embassy of Ireland in Tanzania, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa maziwa na kuinua kipato cha wafugaji nchini