IMANI NI MFUMO WA KURATIBU NGUVU ZA KIROHO

Katika somo la leo tunaingia katika kiwango cha juu zaidi cha uelewa wa imani. Tunajifunza kwamba imani si tu hali ya kuamini moyoni, bali ni mfumo wa kiroho unaoratibu na kuvuta nguvu za Mungu katika maisha ya mwanadamu. Kupitia Mathayo 9:18–22, tunaona wazi kwamba si kila aliyekuwa karibu na Yesu alipokea, lakini yule aliyekuwa na imani ndiyo alivuta nguvu ya uponyaji. Hii inatufundisha kwamba nguvu ya Mungu ipo tayari, lakini inahitaji mfumo sahihi wa kuipokea na mfumo huo ni imani. Katika somo hili utajifunza: Imani kama daraja kati ya mwanadamu na nguvu za Mungu Tofauti kati ya kugusa na kuvuta nguvu ya Mungu Mahali ambapo nguvu za Mungu zipo na namna zinavyojibu imani Jinsi ya kuamsha utendaji wa Mungu katika maisha yako Ujumbe mkuu: Imani yako si ya kukufanya tu umsogelee Mungu ni ya kuvuta mbingu kujibu. Jiunge nasi katika mafundisho haya yenye kina, uamsho, na ufahamu unaobadilisha maisha. 🔴 Join us LIVE on YouTube Search: Voice of Hope #VoiceOfHope #PastorG #Imani #FaithInAction #Mathayo9 #ChristianTeaching #Gospel #SpiritualGrowth #LiveService #YouTubeLive