WAJANE WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Halmashauri ya Jiji la Tanga, kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii, imeungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Wajane Duniani kwa kufanya maandamano makubwa yaliyolenga kuongeza uelewa wa jamii na kutetea haki za wanawake waliofiwa na wenza wao. Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga ambae ndio Mgeni rasmi katika tukio hilo, amewataka wanawake hao walioondokewa na wenza wao kuchangamkia fursa ya upendeleo wa Serikali katika kuwapa kipaumbele wanawake hususani katika asilimia4 zitokanazo mkopo wa asilimia10 unaotewa na Halmashauri zote Nchini Aidha kwa upande wake Bertha Damas ambae ni Afisa Maendeleo ya Jamii Jiji la Tanga amewataka wajane kusimama imara, kujituma, na kuachana kabisa na mtazamo hasi unaowaaminisha kuwa kuondokewa na mume ndio mwisho wa mafanikio na ustawi wa maisha yao. Hata hivyo Bertha amesema changamoto kubwa inayowakabili wajane wengi sio tu changamoto za kiuchumi bali ni mtizamo wa kisaikolojia unaotokana na mifumo ya kijamii inayomkariri mwanamke kama mtu tegemezi wakati wote.