UKARABATI MAABARA WAWAVUTIA WANASAYANSI NGUVUMALI.

Mkuu wa Shule ya sekondari Nguvumali, Mwl. Mkodo Philip, amesema kumekuwa na ongezeko la wanafunzi kusoma masomo ya sayansi baada ya serikali kukarabati maabara shuleni hapo. Amesema kuwa katika shule hiyo maabara zilizokamilika hadi sasa ni mbili mbayo ni ya somo la fizikia na ya kemia, wakati maabara moja ya biologia ipo katika hatua za mwisho kukamilika. "Toka tumeamza kukamilisha hizi maabara tumeona zimeleta mwamko mkubwa kwa watoto wengi kupenda kusoma masomo ya sayansi, na watoto wengi wanasoma masomo ya sayansi kwa sababu sasa wanaziona maabara na facilities zipo" Mwalimu Philip, Mkuu wa Shule ya Sekondari Nguvumali.