Baada ya UDOM kusitisha udahili kwa kozi za ualimu, wadau wapaza sauti

Baadhi ya wadau wa elimu nchini wameeleza wasiwasi wao juu ya uamuzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kusitisha udahili wa wanafunzi katika takribani kozi 11 za ualimu, wakisema hatua hiyo inaweza kuleta athari za upungufu wa walimu nchini katika miaka ijayo. Maoni hayo yametolewa kufuatia tangazo lililotolewa na UDOM kupitia tovuti yake rasmi siku ya Ijumaa, likieleza kuwa kozi hizo hazitapokea wanafunzi katika mwaka wa masomo 2025/2026. Wadau hao wanashauri mamlaka husika kufuatilia kwa karibu athari za uamuzi huo kwa mustakabali wa sekta ya elimu, hususan katika kipindi ambacho nchi inahitaji walimu wenye ujuzi wa kutosha ili kuinua viwango vya elimu. #azamnewsupdates Mhariri| @official_jennifersumi