UCHAGUZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI HORIZON INSTITUTE OF TECHNOLOGY
Ndg. Abdulatif Khamis Faki amechaguliwa kuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Horizon Institute of Technology baada ya kuibuka mshindi katika uchaguzi uliofanyika chuoni hapo, Kijambia, Wilaya ya Magharibi "A", Mkoa wa Mjini Magharibi. Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Mohamed Issa Abdalla, amesema jumla ya kura 441 zilipigwa, ambapo Abdulatif Khamis Faki alipata kura 146 na kutangazwa rasmi kuwa Rais mteule wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho. Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, Abdulatif amesema atatekeleza ahadi alizozitoa wakati wa kampeni kwa kushirikiana na uongozi wa chuo kuboresha mazingira ya kujifunzia, kuimarisha ustawi wa wanafunzi na kuhakikisha elimu yenye ubora inaendelea kutolewa. Kwa upande wao, wagombea wenzake wa nafasi ya urais, Ndg. Aisha Saleh Said na Ndg. Mshibe Ali Haji, wamempongeza rais mteule na kueleza utayari wao wa kushirikiana naye katika kutekeleza maslahi ya wanafunzi na maendeleo ya chuo. Naye Makamu Mkurugenzi wa Horizon Institute of Technology, Yussuf Hamad Omar, amesema uongozi wa chuo utaendelea kushirikiana na serikali ya wanafunzi ili kujenga mazingira bora ya kujifunzia na kuwajengea wanafunzi maarifa na ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira. #Zanzibar #HorizonInstitute #Uchaguzi #SerikaliYaWanafunzi #Elimu #Vijana #AsamOnlineTV #TrendingNow

DC SAID HAJI MRISHO AKAGUA KARO LINALOVUJISHA MAJI MACHAFU FORODHANI

UPDF Delivers on Promise as Museveni’s Wapakhabulo College Pledge Takes Shape

UJENZI WA BARABARA YA MALAWI–KINAZINI KUANZA JULAI 10 KUBORESHA USAFIRI ZANZIBAR

ስነ ስርዓት ምምራቕ መበል 38 ዙርያ ኣባላት ሃገራዊ ኣገልግሎት - ሳዋ | ERi-TV

Cooking A Massive Lamb Pilaf For a Mountain Village Feast!

WAZIRI RAHMA ASITISHA UJENZI KATIKA ENEO LENYE MGOGORO KIZIMKAZI

How Rwandan Refugees SECRETLY Built a Rebel Movement in Uganda & Kenya | Tharcisse Karugarama

Air Tanzania Cockpit Boeing 767-300 Freighter to Kinshasa

MFUMKO WA BEI ZANZIBAR WAPANDA KUTOKA ASILIMIA 4.09 HADI 6.01 MWEZI JUNI 2026

From Minnesota to Dandora dumpsite: The story of an American citizen abandoned in Kenya at just 13.

DC SAID AWATOA HOFU WAVUVI WA MARUHUBI KUHUSU UHAMIAJI NGALAWA

ZAIDI YA MILIONI 200 KUTUMIKA KATIKA UJENZI WA JENGO LA GHOROFA LA TAWI LA CCM - JANG'OMBE

ZAIDI YA NCHI 20 KUSHIRIKI KONGAMANO LA KIMATAIFA LA MAFUTA, NISHATI NA GESI ZANZIBAR

OTHMAN MASOUD AJILIPUA MBELE YA RAIS SAMIA ATOA TAMKO KWA TUNDU LISSU NA WAFUASI WAKE | KATIBA MPYA

Man Renovates ABANDONED STONE HOUSE in 3 years and Gives it a New Life

John Mearsheimer: “Enormous Damage” of U.S.’s Iran War Loss

Amazing Toilet Bowl Manufacturing Process | How Toilet Bowls Are Made in Factory

I might not even be alive before the next election - Peter Obi

Ikiganiro Serguei Lavrov n'Umushikiranganji Édouard Bizimana bagiranye n'Abamenyeshamakuru

