MAKALA FUPI KUHUSU HISTORIA YA MJI WA DODOMA

Karibu katika makala fupi ya historia ya Jiji Kuu la Tanzania: Dodoma Historia yake kwa ufupi, Dodoma, ni jiji kuu la Tanzania, lina historia ya kipekee na ya kuvutia inayochanganya maendeleo ya kisiasa, kijamii, na kiutawala. Licha ya kuwa mji wa kati usio mkubwa sana kwa idadi ya watu ukilinganishwa na Dar es Salaam, Dodoma ni kitovu cha maamuzi ya kitaifa na kisiasa. ASILI ya jina na maeneo yake maarufu huongeza ukubwa na thamani ya jiji hili. Jina "Dodoma" linatokana na neno la lugha ya Kigogo "Idodomya," linalomaanisha "mahali palipoanguka ndizi." Hadithi ya kale inasema kuwa wakati wa karne ya 19, msafara wa wafanyabiashara wa Kiarabu umekuwa ukipita eneo hilo na katika harakati zao, gunia la ndizi kupelekea kuanguka. Tangu hapo, eneo hilo kuanza kujulikana kwa jina hilo. Dodoma ni nyumbani kwa wale wote wa kabila la Wagogo, kabila ambalo limeishi maeneo haya kwa karne nyingi. Kabla ya ukoloni, eneo hili limejulikana kwa kilimo na ufugaji pamoja na tamaduni za Kitanzania zikihifadhiwa kwa umakini mkubwa. Katika miaka ya mwanzoni ya 1900, wakati wa utawala wa Kijerumani, Dodoma imeanza kupata umaarufu zaidi kutokana na ujenzi wa reli ya kati (Central Line Railway) ikiunganisha Dar es Salaam na Kigoma. Reli hiyo imepita katikati ya mji wa Dodoma, na hivyo kuufanya kuwa eneo muhimu la kimkakati kwa usafirishaji na biashara. Mpaka kufikia Mwaka 1973, serikali ya awamu ya kwanza chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikatangaza uamuzi wa kuhamishia makao makuu ya serikali kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma. Lengo kuu ni kuhamasisha maendeleo ya ndani ya nchi (decentralization), kuendeleza maeneo ya kati na pia kuwa karibu zaidi na wananchi wote wa Tanzania, kwa sababu Dodoma iko katikati ya nchi. Hata hivyo, utekelezaji wa mpango huu umekuwa wa taratibu kwa sababu ya changamoto za miundombinu, rasilimali na mahitaji ya mabadiliko ya taasisi za serikali.