BARABARA YA UKUTINI PEMBA MAOMBI YA WANANCHIWALIYOOMBA KUJENGEWA BARABARA KATIKA MAENEOMBALI MBALI.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapimduzi Dk,Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imeamua Kuongeza idadi ya barabara zitakazojengwa Kwa kiwango cha Lami Hadi kufikia Kilomita 300 Mijini na Vijini.. Rais Dk, Mwinyi ametoa tamko hilo alipoifungua Barabara ya Ukutini -Bandarini Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba . DK, Mwinyi ameeleza kuwa Uamuzi huo umefikiwa na Serikali Kufuatia Kuongezeka kwa Maombi ya Wananchi waliyoomba Kujengewa Barabara katika Maeneo mbali mbali. Amefahamisha kuwa Serikali imevuka lengo la Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 ilioainisha Ujenzi wa Kilomita 275 za barabara. Akizungumzia barabara ya Ukutini -Mtangani Bandarini alioifungua Amesema ni hatua Muhimu ya Kufungua fursa za Kiuchumi na kuimarisha fursa za kijamii. "Tutakuwa tumewagusa Wananchi kwani Barabara ni Uchumi" alisisitiza Dk,Mwinyi. Amefahamisha Kuwa mbali na Usafiri barabara hiyo ya Ukutini - Bandarini itafungua Fursa za Ajira kwa kuwa Kuna Bandari na Hoteli katika Eneo hilo pamoja kurahisisha Upatiikanaji wa huduma za kijami ikiwemo Hospital , Skuli na Usafirishaji Rais Dk,Mwinyi ameeleza kuwa Mkataba wa Wananchi na Serikali yao ni Ilani ya Uchaguzi hivyo kuna kila sababu ya kujivunia kwa yote yaliofanyika Katika Ujenzi wa Barabara. Rais Dk, Mwinyi ameipongeza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa Usimamizi Mzuri wa Ujenzi wa Barabara Vijijini na Mijini Unguja na Pemba. Ufunguzi wa Barabara hiyo kunakamilisha Idadi ya Kilomita 85.5 za Barabara zilizojengwa katika Mkoa wa Kusini Pemba. Naye Waziri wa Ujenzi ,Mawasilaino na Uchukuzi Dk,Khalid Salum Muhammed amewahakikishai Wananchi kuwa Serikali haina Unaguzi katika Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo hususan Ujenzi wa Barabara na kwamba zote za Mkoa wa Kusini Pemba ziliyomo katika Mpango wa Ujenzi zitajengwa kwa Awamu . Barabara ya Ukutani - Bandarini yenye Kilomita 4.6 iliojengwa na Kampuni ya IRIS Inakisiwa kugahrimu Dola Millioni 2.658 ni miongoni mwa Mradi wa Ujenzi wa Barabara za Ndani zenye Urefu wa Kilomita 275 .9.

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID
▶︎

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID

Mapokezi ya Waziri wa Mafuta Pemba
▶︎

Mapokezi ya Waziri wa Mafuta Pemba

HATUWEZI KUJENGA BARABARA KIWANGO CHA LAMI   HALAFU TAA ZITUSHINDE" ALISEMA DK, MWINYI PEMBA
▶︎

HATUWEZI KUJENGA BARABARA KIWANGO CHA LAMI HALAFU TAA ZITUSHINDE" ALISEMA DK, MWINYI PEMBA

HOTUBA YA MHE. OTHMAN MKUTANO WA HADHARA GOMBANI PEMBA
▶︎

HOTUBA YA MHE. OTHMAN MKUTANO WA HADHARA GOMBANI PEMBA

Jazira, Kitwana wajichanganya, OMO awakaanga hadharani | GUMZO LA LEO
▶︎

Jazira, Kitwana wajichanganya, OMO awakaanga hadharani | GUMZO LA LEO

Tanzania yapiga marufuku mikutano ya kisiasa. Katika Dira ya Dunia TV
▶︎

Tanzania yapiga marufuku mikutano ya kisiasa. Katika Dira ya Dunia TV

UPASUAJI WA MIDOMO WAZI KATIKA HOSPITALI YA ABDALLAH MZEE PEMBA IMEANZA RASMI LEO
▶︎

UPASUAJI WA MIDOMO WAZI KATIKA HOSPITALI YA ABDALLAH MZEE PEMBA IMEANZA RASMI LEO

#LIVE: KUAPISHWA KWA DK MWINYI ZANZIBAR
▶︎

#LIVE: KUAPISHWA KWA DK MWINYI ZANZIBAR

(SIRI) PEMBA ILITUKUZWA NA MITUME WA ALLAH (SEMA NASI)
▶︎

(SIRI) PEMBA ILITUKUZWA NA MITUME WA ALLAH (SEMA NASI)

Jionee Uzuri wa Kisiwa cha Misali Pemba Chenye Uoto wa Asili na Kinavovutia #MISALI_ISLAND #PEMBA
▶︎

Jionee Uzuri wa Kisiwa cha Misali Pemba Chenye Uoto wa Asili na Kinavovutia #MISALI_ISLAND #PEMBA

KUMECHEMKA🔥 Angry Murkomen sends a FRESH WARNING to Gachagua on Goons in Protests & Maandamano 2027
▶︎

KUMECHEMKA🔥 Angry Murkomen sends a FRESH WARNING to Gachagua on Goons in Protests & Maandamano 2027

🔴TSC: CHAKECHAKE CITY TOUR IN PEMBA ZANZIBAR | A DAY IN EPISODE 13
▶︎

🔴TSC: CHAKECHAKE CITY TOUR IN PEMBA ZANZIBAR | A DAY IN EPISODE 13

BREAKING NEWS: Listen to What Gachagua said after Ndindi Nyoro ADDRESS TO THE NATION
▶︎

BREAKING NEWS: Listen to What Gachagua said after Ndindi Nyoro ADDRESS TO THE NATION

UTENZI ULIOMFURAHISHA RAIS MWINYI KATIKA KILELE CHA KUTIMIZA MIAKA MIWILI YA  MADARAKANI
▶︎

UTENZI ULIOMFURAHISHA RAIS MWINYI KATIKA KILELE CHA KUTIMIZA MIAKA MIWILI YA MADARAKANI

#EXCLUSIVE: JECHA ALIVYOFUTA UCHAGUZI 2015, MKURUGENZI ZEC afunguka "HAKUONEKANA MAENEO YA WAZI"
▶︎

#EXCLUSIVE: JECHA ALIVYOFUTA UCHAGUZI 2015, MKURUGENZI ZEC afunguka "HAKUONEKANA MAENEO YA WAZI"

Haya ndio maeneo ya Kengeja Pemba @discoverzanzibar 2025
▶︎

Haya ndio maeneo ya Kengeja Pemba @discoverzanzibar 2025

#live: UFUNGUZI WA SKULI YA OLE PEMBA.
▶︎

#live: UFUNGUZI WA SKULI YA OLE PEMBA.

🔴 #ZBCLIVE:-MAPOKEZI YA MGOMBEA MTEULE WA URAIS WA ZANZIBAR 2025 KUPITIA CCM DKT .HUSSEIN ALI MWINYI
▶︎

🔴 #ZBCLIVE:-MAPOKEZI YA MGOMBEA MTEULE WA URAIS WA ZANZIBAR 2025 KUPITIA CCM DKT .HUSSEIN ALI MWINYI

RAIS DKT. MAGUFULI AKIWA NJIANI KUELEKEA JIJINI DODOMA
▶︎

RAIS DKT. MAGUFULI AKIWA NJIANI KUELEKEA JIJINI DODOMA

MAKAMO WA PILI KUTORIZISHWA NA UJENZI WA BARABARA PEMBA
▶︎

MAKAMO WA PILI KUTORIZISHWA NA UJENZI WA BARABARA PEMBA