KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID NI UTANI WA KISHERIA: ACT WAZALENDO TUNATAKA TUME YA BARAZA LA WAWAKILISHI ICHUNGUZE UTOAJI HOLELA WA UZANZIBARI. Zanzibar, Juni 24, 2026 Hivi karibuni, kumekuwepo na mjadala mzito ndani na nje ya Baraza la Wawakilishi kuhusu hadhi, haki, na ulinzi wa Mzanzibari ndani ya nchi yake. Katika hali ya kusikitisha, umma umeshuhudia kauli nyepesi kutoka kwa Mawaziri wa Serikali, wakidai kuwa mtu yeyote anaweza kuwa Mzanzibari na kupewa Kitambulisho cha Mzanzibari (ZAN ID) ilimradi tu ameishi Zanzibar kwa muda wa miaka kumi (10). Kama Mwanasheria Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, ninalazimika kutoa ufafanuzi wa kisheria na kisiasa ili kuwapa changamoto mawaziri hao na kuikumbusha Serikali kuwa Uzanzibari na asili ya nchi hii sio bidhaa ya sokoni inayoweza kugawiwa kwa matamshi ya kisiasa majukwaani. Uzanzibari hauanzi wala hauishii kwenye kupata karatasi ya ZAN ID; una misingi mikali ya kihistoria, kisheria, na kikatiba. 1. Msingi wa Kikatiba: Kulinda Historia na Urithi wa Zanzibar Kwanza, ni lazima Serikali ikumbushwe kuwa ulinzi wa utambulisho wa Mzanzibari una baraka kamili ya Katiba yetu. Ibara ya 6 ya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984 inaweka wajibu wa kikatiba wa kulinda, kuendeleza, na kuhifadhi historia, utamaduni, na urithi wa Zanzibar. Urithi huo unajumuisha watu wake na haki zao za asili. Tunataka iwe wazi mbele ya umma kuwa Sheria hizi hazikuwekwa kwa lengo la kuwabagua au kuwachukia ndugu zetu wa Tanzania Bara/Tanganyika au mtu yeyote kutoka nje ya Zanzibar. Hapana! Zanzibar ni nchi ya ukarimu na udugu. Hata hivyo, kama ilivyo katika maeneo yote yenye mamlaka ya ndani duniani, sheria hizi zipo kisheria kwa ajili ya kulinda historia, hadhi, na heshima ya nchi na kuhakikisha rasilimali zilizopo (kama vile ardhi na nafasi za ajira) zinalindwa kwa maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo. Ndivyo pia ilivyo kwa Zanzibar – na makhsusi kabisa kwa kuwa Zanzibar yetu ni nchi ya visiwa. Ardhi yake haitanuki. Rasilimali zake haziongezeki. Duniani kote utaratibu huu upo na unaheshimika. Kwa mfano, Katika muundo wa Kikatiba wa nchi ya China na Jimbo la Hong Kong, ingawa Hong Kong ni sehemu kamili ya mamlaka ya China, raia yeyote wa China Bara (Mainland China) hawezi kuwa mkaazi wa kudumu wa Hong Kong au kupata Haki za Kipekee za eneo hilo (kama kupiga kura, kupata makaazi au kufanya kazi bila ya kibali maalum) kwa kigezo cha utaifa wake tu wa Uchina. Lazima akidhi sheria na vigezo vikali vya ndani vya Hong Kong. Kama nchi kubwa na zenye nguvu duniani zinalinda maeneno yao ya ndani kisheria ili kuzuia mifumo yao isizidiwe, iweje hapa Zanzibar viongozi wetu waone kulinda sheria zetu ni ubaguzi au fitina za kuvunja Muungano? 2. Swali kwa Waziri: "Kama Muungano ni Maisha, Uzanzibari ni Nini?" Wakati akizungumza Barazani, waziri mwenye dhamana Tawala za Mikoa na Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia suala la ZAN-ID liko chini yake, Bwana Idrissa Kitwana na wajumbe wengine, walijaribu kujivika mwavuli wa uzalendo kwa kudai kuwa watu wanaozungumzia hoja ya Uza

SEREKALI RASMI YAFUNGA HOJA ZA MJADALA WA UBAGUZI ZILIZO IBUKA ZANZIBAR NA TANZANIA BARA

Leo #MariaSpaces tunajadili: Ukweli, Haki na Uwajibikaji kama dai kubwa la 7/7 - tuko tayari?

Jeffrey Sachs LIVE | Jeffrey Sachs Tears Into Trump, Makes Shocking Prediction on Middle East War

Zanzibar Ministers must stop using the Union as an excuse for intimidation – ACT

ACT WAFUNGUKA AJIRA ZA WAZANZIBAR, WATAKA VIJANA KUPEWA KIPAUMBELE! 🔥

MKITOKA KUFANYA VURUGU TUTAKATANA MIGUU, TUNA VIJANA WAKUTOSHA MSITHUBUTU, SHEIKH MWAIPOPO

Insecurity: It's Time Nigerians Armed Themselves; Tinubu Spends $150m To Stop Trump

Qui a tué Monferrier Dorval ? Les zones d'ombre d'un crime d'État

Nigeria Strikes Back: The South Africa Crisis Just Went Continental

WATCH How Lawyer Martin Kpebu And Lawyer Edudzi Tamaklo Dealt With Wontumi's Lawyer, Appiah Kubi

MWALIMU ASIMULIA ALIVYOKATWA MKONO NA MUMEWE, WATOTO WAKE WAONE VIDOGOLE VILIVYOKATWA, WANAFUNZI

ACT WAZALENDO CONFRONTS KITWANA WITH TOUGH QUESTIONS ON THE UNION, "TALKING ABOUT ZANZIBARI IDENT...

If you are not afraid, mention Kennedy Agyapong's name - Bernard Baidoo to Dr Zaato

MIRAJI|UBINGWA WA YANGA MSIMU HUU UNA THAMAN KULIKO ILE MINNE|SIMBA TUNASHINDA ILA LIGI IMESHAISHA

Urgent : Ousmane Sonko humilie Abdou Mbow "sa wayy togal té noppi"

ජනතා ජයග්රහණයක්. පාර්ලිමේන්තු සම්ප්රදාය නොදන්නා ආණ්ඩුව වැට් බදු යෝජනා හකුළා ගනී.

RAIS MWINYI: TEHAMA MAHAKAMANI IHARAKISHE HAKI, MASAJU ASIFIA UJENZI WA MAHAKAMA PEMBA 🔥

Trump Sends Vance to Concede to Iran & Reflecting Pool Is Filled with Corruption | The Daily Show

MOTO JE, UNAMJUA NCHIMBI? SAFARI YA KIONGOZI MWENYE USHAWISHI MKUBWA CCM

