TFRA YATOA MAFUNZO KWA MAAFISA KILIMO MOSHI DC
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), imetoa semina kwa Maafisa Kilimo wa wilaya, kata na vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi kwa lengo la kuboresha utoaji wa elimu sahihi kuhusu matumizi ya mbolea pamoja na uhuishaji wa taarifa za wakulima katika maeneo yao ya kazi. Semina hiyo imetolewa na Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa TFRA, Gothard Liampawe, ambaye amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo maafisa kilimo na kuwapatia uelewa sahihi kuhusu namna mfumo wa taarifa za wakulima unavyofanya kazi ili kusaidia upatikanaji wa takwimu sahihi. Amesema takwimu sahihi za wakulima ni muhimu katika kupanga mipango ya maendeleo ya sekta ya kilimo na kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo kwa wakati. “Tunapowajengea uwezo maafisa kilimo, tunahakikisha taarifa sahihi zinawafikia wakulima na pia serikali inapata takwimu sahihi zitakazosaidia kupanga mipango ya kuboresha uzalishaji wa mazao,” amesema Liampawe. Kwa upande wake Mratibu wa Pembejeo za Ruzuku wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Hamza Mwinyihija, amesema halmashauri imejipanga kuhakikisha maafisa kilimo wanatoa elimu sahihi kwa wakulima kuhusu uhuishaji wa taarifa zao pamoja na matumizi bora ya mbolea ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao. “Ni wajibu wa maafisa kilimo kuwafikia wakulima katika maeneo yao na kuwapa elimu sahihi kuhusu matumizi ya mbolea na umuhimu wa kuhuisha taarifa zao ili waweze kunufaika na programu mbalimbali za serikali,” amesema Mwinyihija. Aidha, amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya maafisa kilimo na wakulima utasaidia kuboresha mfumo wa usimamizi wa pembejeo na kuongeza ufanisi katika sekta ya kilimo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

MOSHI DC NA BODI YA KAHAWA KUSAMBAZA MICHE ZAIDI YA MILIONI 1 KUFUFUA KILIMO CHA KAHAWA

WATUMISHI MOSHI DC WASHIRIKI KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA, WAHIMIZWA KUCHEZA MICHEZO,WAIMBA NA KUCHEZA

How China–Kenya cooperation is transforming agriculture

KARAGWE DC KUJENGA SOKO LA KISASA...

ODM at a crossroads | Suba South MP Caroli Omondi speaks ahead of NDC showdown

I refused to sell Wambugu apple business to a white man for 30M, today it’s worth billions | LNN

VIDEO: MOSHI DC YATOA MAFUNZO KWA VIKUNDI 46, YATENGA MIL 477.4 KUWEZESHA MIKOPO

MOSHI DC WAJITATHIMINI, WAJIPANGA KUINUA TAALUMA NA KUBORESHA UFAULU 2026

DIWANI AIBUA CHANZO KIPYA CHA MAPATO, NI MAPOROMOKO YA MAJI YA KITORO, WATAALAMU WAFANYA TATHIMINI

"We Will Open Africa" — A Conversation with Aliko Dangote

Tuko Kadi: How Kenyan GenZs Are Mobilising To Register As Voters | Allan Ademba

ውሀ ፣መሬት እና ወጣቶችን ያገናኘው የበጋ መስኖ በቸሀ ወረዳ | ወደገጠር |EBC | EBCDOTSTREAM

DCC MOSHI YABARIKI KUANZISHWA KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA VUNJO

Tracking Kenya's Growing Debt | Drunken Lectures

How Traoré Just Broke Africa’s Most Profitable Scam

MOSHI DC BUILDS CAPACITY FOR SCHOOL HEADS, PURCHASING TEACHERS TO MANAGE PURCHASES AND SUPPLY EFF...

PROF OMAR WA ACT WAZALENDO AISHAMBULIA OFISI YA MAKAMO WA PILI WA RAIS

MAFUNZO YA CHANJO YAWAJENGEA UWEZO WAUGUZI WASAIDIZI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA JAMII MOSHI DC

Grass to Gold! Revolutionizing Livestock Feed: Juncao Grass Technology in Kenya!

