DKT. MWINYI AKUTANA NA MHAMASISHAJI WA DHANA YA UTALII HALALI DUNIANI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Mwanazuoni na Mhamasishaji wa Dhana ya Utalii Halali Duniani, Bw. Ismail Bullock kutoka Dubai, katika mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Zanzibar. Bw. Bullock alifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha kwa Rais pamoja na ujumbe alioambatana nao kutoka Taasisi ya Samia Foundation. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Mwinyi amesifu juhudi zinazofanywa na mwanazuoni huyo katika kuutangaza na kuhamasisha utalii halali katika mataifa mbalimbali duniani, akieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaunga mkono jitihada hizo za kukuza na kuendeleza utalii unaozingatia misingi ya Kiislamu. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema Zanzibar inaendelea kuimarisha sekta ya utalii kwa kuzingatia mahitaji ya makundi mbalimbali ya watalii, ikiwemo wale wanaopendelea huduma zinazokwenda sambamba na maadili na misingi ya dini ya Kiislamu. Kwa upande wake, Bw. Ismail Bullock amesema dhamira yake ni kuona dhana ya utalii halali inaeleweka na kutekelezwa katika mataifa mbalimbali duniani, akibainisha kuwa dhana hiyo imeendelea kupata umaarufu mkubwa katika nchi nyingi. Amesema akiwa Zanzibar ameendelea kutoa mafunzo kwa wadau wa sekta ya utalii kuhusu umuhimu wa utalii halali na namna unavyoweza kuchangia ukuaji wa sekta hiyo pamoja na kuongeza fursa za kiuchumi. #Zanzibar #UtaliiHalali #HalalTourism #DktMwinyi #IsmailBullock #Tourism #SamiaFoundation #Utalii #ASAMOnlineTV #BreakingNews

KUHUSU KAULI YA MHE. SIMAI, WATU WASIKUZE MAMBO, TUTAMWITA ATUSAIDIE HAO WASALITI: KOMRED MBETO

DC MJINI AKAGUA HUDUMA HOSPITALI YA LUMUMBA, ASISITIZA UFANISI NA HUDUMA BORA

KIJANA APORWA ZAIDI YA MILIONI 10 BAADA YA KUVAMIWA NA WATU WASIOJULIKANA

DHAMIRA YA DK.MWINYI KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI INAONEKANA KIVITENDO

BALAA LA MHe, Jaku ATAJA MADANGURO YA KUJIUZA YALIPO YOTE

RAIS MWINYI AWAALIKA WAWEKEZAJI WA KIARABU ZANZIBAR, ASEMA FURSA NI NYINGI NA MAZINGIRA NI RAFIKI

HILI NDIO DARAJA REFU ZAIDI ZANZIBAR

NAIBU SHEHA ASIMAMISHWA KAZI KWA UUZAJI WA MAENEO YA HIFADHI - PAJE

Waliopata ajali ya Meli waokolewa. #views #foryou #zanzibar #tanzania

''uso umeumbwa na haya'' JAKU ALIVYOKUA MPOLE LEO BARAZANI

EXCLUSIVE: AMANI KARUME ATEMA CHECHE, AFUNGUKA SAKATA LA BANDARI

ALI KARUME AIBUA MAPYA, ASEMA CCM HAIJAWAHI KUSHINDA UCHAGUZI ZANZIBAR, WANAKAA MADARAKANI KWA UBABE

MADEREVA ZANZIBAR WAFUNGULIWA FURSA MPYA ZA AJIRA

EMBE ZA MUYUNI ZANZIBAR ZAZUA BALAA ''utakachojibiwa hukitaki, una majibu Mfukoni''

JANG'OMBE BADO YAENDELEA KUSUKWA NA KING

MAJI TAKA, GUMZO HOSPITALI YA WILAYA CHUMBUNI

MJI MKONGWE KUMEKUCHA WAVAMIA MAENEO KUHUSU USAFI

Visiting the Muslim Island with over 8000 Mosques Lombok Indonesia 🇮🇩

RAIS DKT. MWINYI AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WA NCHI ZA KIARABU KUWEKEZA ZANZIBAR

