RAIS DKT. MWINYI AWAKARIBISHA WAWEKEZAJI WA NCHI ZA KIARABU KUWEKEZA ZANZIBAR
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amewakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka nchi za Kiarabu kuwekeza Zanzibar, akibainisha kuwa Zanzibar ina mazingira bora na fursa nyingi za uwekezaji katika sekta mbalimbali za maendeleo. Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Ikulu Zanzibar alipokutana na Mabalozi wa nchi za Kiarabu wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania, waliofika kwa ajili ya kumsalimia pamoja na kumpongeza kwa hatua kubwa ya maendeleo inayofikiwa na Zanzibar hivi sasa. Amesema Zanzibar inaendelea kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji kupitia maboresho ya miundombinu, sera rafiki za uwekezaji pamoja na kuimarika kwa huduma mbalimbali zinazowawezesha wawekezaji kufanya shughuli zao kwa ufanisi. Aidha, amezipongeza nchi hizo za Kiarabu kwa kuendelea kuimarisha uhusiano wake na Tanzania, ikiwemo Zanzibar, pamoja na mchango wao katika kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Kwa niaba ya Mabalozi hao, Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, Mhe. Yahya Ahmed Okesh, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa uongozi wake ulioleta maendeleo makubwa katika uchumi wa Zanzibar, miundombinu na ustawi wa wananchi. #Zanzibar #Uwekezaji #DktHusseinMwinyi #NchiZaKiarabu #Maendeleo #ASAMOnlineTV

DKT. MWINYI ATANGAZA MAPINDUZI YA UCHUMI! ZANZIBAR YAFUNGUA MILANGO KWA WAWEKEZAJI DUNIANI

#KUMEKUCHA: JAKU ACHAGA BARAZANI ''sizungumzi kihindi '' ATAKA MAJIBU

DC MJINI AKAGUA HUDUMA HOSPITALI YA LUMUMBA, ASISITIZA UFANISI NA HUDUMA BORA

MTAFARUKU: Wazanzibari Wawachonokoa Watanganyika

🔴 #ZBCLIVE :- BARAZA LA 11 LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR - MKUTANO 03 KIKAO CHA 31

BAADA YA KUPOKEA NDEGE ZNZ RAIS MWINYI ATOA MAAGIZO KWA ATCL NDEGE ZIONGEZE SAFARI

JAKU AJIRIPUA KWA NAIBU WAZIR BADRIA ''TUFUTANE UKAONE USHAHIDI WA KINYAMWEZI''

KIJANA APORWA ZAIDI YA MILIONI 10 BAADA YA KUVAMIWA NA WATU WASIOJULIKANA

Rais wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) atembelea Zanzibar

NAIBU SHEHA ASIMAMISHWA KAZI KWA UUZAJI WA MAENEO YA HIFADHI - PAJE

UFAHAMU MRADI WA BANDARI YA MPIGA DURI

HECHE AMCHANA SAIDI ISSA MOHAMED AMUITA MSALITI SIO MWENZETU | ANATUMIKA ALIFUNGUA KESI YA UONGO.

TAZAMA MAHUJAJ WA KENYA WAKIREGEA BAADA YA HAJJ

🔴 #ZBCLIVE :- BARAZA LA 11 LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR - MKUTANO 03 KIKAO CHA 29

Hii ni Zanzibar maeneo kutokea Michenzani Kijangwani Mwembeladu hadi Amani @discoverzanzibar

HOJA NZITO ZAIBUKA DKT RIZIKI APANGUA HOJA ZA PROF OMAR FAKIH BARAZA LA WAWAKILISHI

MADEREVA ZANZIBAR WAFUNGULIWA FURSA MPYA ZA AJIRA

KAULI YA ZFDA KUHUSU USALAMA WA CHAKULA - ZANZIBAR

MJI MKONGWE KUMEKUCHA WAVAMIA MAENEO KUHUSU USAFI

