SERIKALI YAKAGUA MASOKO KATAVI, YASISITIZA USAFI NA BEI STAHIKI ZA BIDHAA.

Serikali ya Mkoa wa Katavi imeendelea kusimamia kwa karibu shughuli za biashara katika masoko, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa bei nafuu. Hayo yamebainishwa leo, Novemba 6, 2025, wakati Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji, Bw. Florence Chrisant, alipongoza timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda katika ukaguzi wa masoko kadhaa ndani ya Manispaa hiyo. Masoko yaliyotembelewa ni Soko Kuu, Soko la Mpanda Hoteli, na Soko la Buzogwe, ambapo timu hiyo ilijiridhisha na hali ya upatikanaji wa bidhaa, mwenendo wa bei pamoja na mazingira ya usafi katika maeneo ya biashara. Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Bw. Chrisant alisema kuwa kwa ujumla hali ya biashara ni nzuri na bidhaa muhimu zinapatikana, ingawa ongezeko la bei ya maji ya kunywa bado lipo. Kwa sasa, chupa kubwa ya maji inauzwa kati ya shilingi 1,500 hadi 2,000, ikilinganishwa na shilingi 1,000 kabla ya kipindi cha uchaguzi. Aidha, alitoa wito kwa viongozi wa masoko kuhakikisha usafi unazingatiwa ipasavyo, akisisitiza kuwa mkoa unaelekea katika msimu wa mvua na matunda, hivyo ni muhimu kuzuia uwezekano wa magonjwa ya mlipuko. Kwa upande wake, Afisa Biashara wa Manispaa ya Mpanda, Bw. Paul Kahoya, alibainisha kuwa changamoto ya maji itapatiwa suluhisho muda si mrefu, kutokana na hali ya usambazaji kuwa imetengemaa na magari ya kusafirisha bidhaa kuruhusiwa kufanya kazi kwa uhuru. Amesema pia kuwa tayari mwekezaji katika eneo la Kakese ameanzisha kiwanda cha maji, kitakachosaidia kupunguza kabisa changamoto ya upatikanaji wa maji mara michakato midogo iliyosalia itakapokamilika. Viongozi wa masoko hayo wamepongeza uamuzi wa serikali kufuatilia kwa karibu shughuli za biashara, wakisema hatua hiyo imeongeza imani, ushirikiano na ari ya kufanya kazi miongoni mwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi.

FULL VIDEO KILICHOMPONZA MWENYEKITI WA MTAA HADI RC CHALAMILA KUAGIZA AKAMATWE | UTAPELI WA VIWANJA.
▶︎

FULL VIDEO KILICHOMPONZA MWENYEKITI WA MTAA HADI RC CHALAMILA KUAGIZA AKAMATWE | UTAPELI WA VIWANJA.

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu
▶︎

AMSHITAKI MMEWE KWA WAZIRI MKUU "ANAJINYEA TU" Wananchi Wavunjika Mbavu

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....
▶︎

CHALAMILA ALIVYOAGIZA MWENYEKITI AKAMATWE na POLISI BAADA ya KUDAIWA KUTAPELI WATU VIWANJA....

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds
▶︎

How China Built an Impossible Bridge Above the Clouds

The Jamaica They Don't Want You To See!
▶︎

The Jamaica They Don't Want You To See!

RC MRINDOKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA MCHEPUO WA KIINGEREZA TANGANYIKA DC.
▶︎

RC MRINDOKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA MCHEPUO WA KIINGEREZA TANGANYIKA DC.

RC MRINDOKO AAGIZA WAFANYABIASHARA KATAVI KUTOPANDISHA BEI WAKATI WA MFUNGO WA KWARESMA NA RAMADHANI
▶︎

RC MRINDOKO AAGIZA WAFANYABIASHARA KATAVI KUTOPANDISHA BEI WAKATI WA MFUNGO WA KWARESMA NA RAMADHANI

WAZIRI MAVUNDE ASITISHA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI WA MADINI BAADHI YA MACHIMBO KATAVI
▶︎

WAZIRI MAVUNDE ASITISHA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI WA MADINI BAADHI YA MACHIMBO KATAVI

JESHI LA UHAMIAJI LATOA MAFUNZO KWA MAAFISA USAFIRISHAJI
▶︎

JESHI LA UHAMIAJI LATOA MAFUNZO KWA MAAFISA USAFIRISHAJI

SADIO MANÉ HUMILIATED BRAZIL AND SENEGAL INJURED THE BRAZILIAN NATIONAL TEAM WITH A HISTORIC DEFEAT!
▶︎

SADIO MANÉ HUMILIATED BRAZIL AND SENEGAL INJURED THE BRAZILIAN NATIONAL TEAM WITH A HISTORIC DEFEAT!

RC MRINDOKO AIPONGEZA TANGANYIKA DC KWA KUTENGA ENEO LA MAONESHO YA NANENANE.
▶︎

RC MRINDOKO AIPONGEZA TANGANYIKA DC KWA KUTENGA ENEO LA MAONESHO YA NANENANE.

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!
▶︎

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!

KESI YA UHAINI YA LISSU YAIBUKA MAPYA, CHADEMA WADAI POLISI WAMEPANGA VURUGU MAHAKAMANI
▶︎

KESI YA UHAINI YA LISSU YAIBUKA MAPYA, CHADEMA WADAI POLISI WAMEPANGA VURUGU MAHAKAMANI

WAZIRI MKUU MHE. DKT. NCHEMBA AKAGUA DARAJA LA SITALIKE, MKOANI KATAVI.
▶︎

WAZIRI MKUU MHE. DKT. NCHEMBA AKAGUA DARAJA LA SITALIKE, MKOANI KATAVI.

WAZIRI MKUU AAGIZA MKANDARASI KUFANYA KAZI USIKU NA MCHANA KUKAMILISHA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATAVI
▶︎

WAZIRI MKUU AAGIZA MKANDARASI KUFANYA KAZI USIKU NA MCHANA KUKAMILISHA JENGO LA MAMA NA MTOTO KATAVI

KATAVI BOYS YAANZA VIZURI UTEKELEZAJI MPANGO WA LISHE BORA KWA KILA MWANAFUNZI SHULENI
▶︎

KATAVI BOYS YAANZA VIZURI UTEKELEZAJI MPANGO WA LISHE BORA KWA KILA MWANAFUNZI SHULENI

SERIKALI MBIONI KUZINDUA KAMPUNI YA MFUKO WA DHAMANA KWA WACHIMBAJI WADOGO
▶︎

SERIKALI MBIONI KUZINDUA KAMPUNI YA MFUKO WA DHAMANA KWA WACHIMBAJI WADOGO

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA KATAVI WAKUMBUSHWA WAJIBU WA KULINDA MALI ZA SERIKALI.
▶︎

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA KATAVI WAKUMBUSHWA WAJIBU WA KULINDA MALI ZA SERIKALI.

MWANAMKE ALIYE MTEKA MTOTO SHULENI NA KUTAKA ALIPWE  MILIONI 20,AKAMATWA NA MTOTO  TABORA
▶︎

MWANAMKE ALIYE MTEKA MTOTO SHULENI NA KUTAKA ALIPWE MILIONI 20,AKAMATWA NA MTOTO TABORA

DC MAULID DOTTO ALISHUKURU SHIRIKA LA COMPASSION KWA KUTOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO
▶︎

DC MAULID DOTTO ALISHUKURU SHIRIKA LA COMPASSION KWA KUTOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO