WALIKOMBOLEWA waimba juu, waki...

307. WALIKOMBOLEWA waimba juu, waki... 307. WALIKOMBOLEWA waimba juu, wakisujudu mbele zake Bwana. Huzuni na taabu za dunia Bwana amewaondolea zote. :/: Wanamwimbia Mwana Kondoo aliyekufa, sasa yu hai, ameyashinda mauti. :/: 2. Wanashika vinubi mikononi wakiimba wimbo wa Mwana Kondoo. Na Musa mtumishi wake Mungu akifurahia matendo yao. 3. Wasiopenda kumsujudia, katika dunia hii ya sasa. Hawataonekana mbele zake, watateketea motoni kweli. 4. Muda unaobaki ni mfupi, tujitayarisheni ndugu sasa. Bwana ajapo tuwepo tayari, tutaimba naye kule mbinguni. Mtungaji hajulikani