SAKATA LA WANAFUNZI KUZUIWA KWENDA LIKIZO WAZIRI WA ELIMU ATOA MAELEKEZO

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amezitaka shule binafsi kuwaruhusu wanafunzi kwenda nyumbani wakati wa likizo kwa ajili ya kupumzika. Waziri Mkenda ametoa maelekezo nje ya viwanja vya Bunge kufuatia malalamiko yaliyotolewa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii juu ya baadhi ya shule kuwazuia wanafunzi kwenda likizo na kuwabakisha shule kwa ajili ya kujisomea na kujiandaa na mitihani. Prof. Mkenda ameongeza kuwa iwapo kuna shule italazimika kuwabakiza wanafunzi wakati wa likizo, kuwepo makubaliano baina ya shule na wazazi. Follow us on: FACEBOOK; SpotiLeo:   / spotileo-176.  . HabariLeo:   / habarileo   DailyNews:   / dailynewstz   INSTAGRAM; HabariLeo: https://instagram.com/habarileo_tz?ig... SpotiLeo: https://instagram.com/spotileo?igshid... TWITTER; Twitter HabariLeo: https://twitter.com/HabariLeo?s=09