BOTI YAZAMA MAJI COCO BEACH TISA WAOKOLEWA

Wavuvi Tisa waliokuwa katika shuguli za uvuvi eneo la Coco Beach wamenusurika kifo baada ya boti yao kuzama maji katika eneo hilo. Mrakibu msaidizi wa Kikosi cha Zimamoto na uokoaji Mkoa wa Zimamoto Kinondoni Elisha Mugisha amesema boti hilo lilizama majira ya mchana, na kwamba jeshi hilo kwa kushirikiana na vijana wa Coco Beach maarufu kama Beach Boys mafunzo maalumu ya uokozi wamefanikiwa kuokoa watu hao.