MWENYEKITI ASIMULIA TUKIO ZIMA POLISI WAWILI WALIVYOUAWA 'NILIPIGIWA SIMU', WALISEMA TUNASHIDA'

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilingo, Kijiji cha Msagali wilayani Mpwapwa, Alex Chikumbi amesimulia ilivyokuwa wakati wa tukio la mauaji ya askari polisi wawili na mtuhumiwa wa unyang'anyi, Atanasio Malenda. Tukio hilo lilitokea Desemba 18, 2024, wakati Koplo Jairo Kalanda na Konstebo Alfred John walipokwenda kumkamata mtuhumiwa huyo. Chikumbi amesema askari walikuwa wamejipanga kumkamata Malenda lakini walipofika eneo la tukio, mtuhumiwa alijaribu kupambana nao. Katika harakati hizo, polisi hao wawili walipoteza maisha pamoja na mtuhumiwa mwenyewe. “Hili lilikuwa tukio la kushtua kijiji chetu. Tulishuhudia jinsi hali ilivyokuwa mbaya na hatutarajii mambo kama haya kutokea tena,” amesema Chikumbi. Tukio hili limeacha simanzi kubwa kwa familia za polisi waliopoteza maisha, huku mamlaka zikiendelea na uchunguzi wa kina kubaini chanzo halisi cha mauaji hayo. Katika tukio hilo, Koplo Msuka na mgambo wa kijiji hicho, Masima Nyau walijeruhiwa na walipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa. Juzi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi alisema askari hao waliuawa walipokuwa kwenye mapambano ya risasi na mtuhumiwa aliyedaiwa kujeruhi na kupora Sh2 milioni. Kamanda Katabazi alisema Malenda alifariki dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa kutokana na majeraha aliyoyapata wakati wa mapambano hayo. Akizungumza na Mwananchi jijini Dodoma leo Desemba 20, Chikumbi amesema saa 1:00 jioni Desemba 17 alipigiwa simu na askari wa upelelezi akimweleza kuna mtuhumiwa aliye kitongojini kwake. Amesema baada ya ujumbe huo, aliwaeleza mbona hamfahamu mtuhumiwa huyo, lakini walimweleza asubiri hadi watakapofika watamueleza. “Nikawahoji je, mtendaji anazo taarifa? wakasema wanampigia simu lakini hapokei. Nilikaa hadi nikasinzia. Waliponipigia nikawauliza tena kama wameshampata mtendaji, walinijibu hapokei,” amesema. “Niliwaambia mtakapokuja mimi mtuhumiwa simjui lakini wao wakasema tutakupa maelekezo kwa upande wa mwenyekiti mwenzako. Nikasema sawa, wakampigia (mwenyekiti wa kitongoji kingine) akasema sawa akawaelekeza (askari)” amemsema. Chikumbi amesema mbali ya maelekezo hayo, mwenyekiti huyo aliwapa kijana ambaye alifika katika kitongoji hicho saa 3:00 usiku akilenga kuwaelekeza polisi nyumbani kwa mtuhumiwa huyo. Amesema alimpigia askari jamii (mgambo) Nyau aliyefika nyumbani kwake na kumwelezea kuhusu tukio hilo, iliwalazimu waambatane na askari kwenda kumkata mtuhumiwa. “Alikwenda kuvaa jaketi na kurudi. Ilipotimia saa 7:00 usiku askari walipiga simu na kumwambia wameshafika kilomita 387, nikawaambia wameshapita wameingia eneo jingine. Niliwaelekeza wakarudi hadi eneo lililoangukia treni,” amesema. Tukio lilivyokuwa Chikumbi amesema walifika askari watano na kijana aliyekuwa akiwaonyesha kwa mtuhumiwa aliwaambia ana nyumba mbili (wake wawili), hali iliyowafanya kujigawa katika makundi mawili.

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG
▶︎

CAG MSTAAFU PROFESA ASSAD AFUNGUKA SABABU ZILIZOPELEKEA KUONDOLEWA KATIKA NAFASI YA CAG

"Mtoto aliacha mlango wazi ili mama yake akirudi asimsumbue kuufungua" Majirani waeleza
▶︎

"Mtoto aliacha mlango wazi ili mama yake akirudi asimsumbue kuufungua" Majirani waeleza

POLISI WAWILI WAUAWA DODOMA WAKIMFUATA MTUHUMIWA
▶︎

POLISI WAWILI WAUAWA DODOMA WAKIMFUATA MTUHUMIWA

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.
▶︎

Historia ya Hayati Luteni Jenerali Silas Mayunga Vita Vya Kagera.

"INAHITAJIKA MIUJIZA" AMRI KIEMBA AITABIRIA TIMU HII UBINGWA LIGI KUU, AMCHAMBUA MVP, MFUGAJI BORA !
▶︎

"INAHITAJIKA MIUJIZA" AMRI KIEMBA AITABIRIA TIMU HII UBINGWA LIGI KUU, AMCHAMBUA MVP, MFUGAJI BORA !

Tanzania yapiga marufuku mikutano ya kisiasa. Katika Dira ya Dunia TV
▶︎

Tanzania yapiga marufuku mikutano ya kisiasa. Katika Dira ya Dunia TV

Where Is She?-Nakuru family's agony deepens as missing daughter Mary Njeri vanishes without a trace
▶︎

Where Is She?-Nakuru family's agony deepens as missing daughter Mary Njeri vanishes without a trace

Babu Owino speaks at Milimani Law Courts after defending 'Mr Speaker Sir' Ezekiel Kyama
▶︎

Babu Owino speaks at Milimani Law Courts after defending 'Mr Speaker Sir' Ezekiel Kyama

Murkomen Asema Ruto Hana Mpinzani... Lakini Video ya WANTAM Yazua Maswali Makubwa
▶︎

Murkomen Asema Ruto Hana Mpinzani... Lakini Video ya WANTAM Yazua Maswali Makubwa

MIILI ASKARI WALIOUAWA KWA RISASI YAAGWA
▶︎

MIILI ASKARI WALIOUAWA KWA RISASI YAAGWA

WAKILI MADELEKA AMSHUKIA WAZIRI ATOE KIFUNGU KILICHOMPA MAMLAKA  KUMUAMRISHA IGP
▶︎

WAKILI MADELEKA AMSHUKIA WAZIRI ATOE KIFUNGU KILICHOMPA MAMLAKA KUMUAMRISHA IGP

SHUHUDA AELEZA POLISI WALIVYOUAWA 'MUUAJI ALIKUWA MZOEFU'.
▶︎

SHUHUDA AELEZA POLISI WALIVYOUAWA 'MUUAJI ALIKUWA MZOEFU'.

BREAKING: Ruto in Shock After Sifuna Takes Over ODM | Boniface's Dream, Rogers Kakasungura
▶︎

BREAKING: Ruto in Shock After Sifuna Takes Over ODM | Boniface's Dream, Rogers Kakasungura

Wanga-Junet WHISKED from Busia Rally as angry Youth STORM the Event amid Ruto Campaign
▶︎

Wanga-Junet WHISKED from Busia Rally as angry Youth STORM the Event amid Ruto Campaign

MIAKA 18 JELA KWA KUSINGIZIWA MAUAJI, ASIMULIA ALIVYOTESWA, AOMBA MSAADA
▶︎

MIAKA 18 JELA KWA KUSINGIZIWA MAUAJI, ASIMULIA ALIVYOTESWA, AOMBA MSAADA

Inama ya Unity Club | Gen (Rtd) Fred Ibingira
▶︎

Inama ya Unity Club | Gen (Rtd) Fred Ibingira

Ajali:Sita wanusurika kifo,Lori likfeli breki Moshi!
▶︎

Ajali:Sita wanusurika kifo,Lori likfeli breki Moshi!

OBINNA SHOW LIVE:  FOR BETTER FOR WORSE - Rigathi Gachagua
▶︎

OBINNA SHOW LIVE: FOR BETTER FOR WORSE - Rigathi Gachagua

Lapolis frape Bandi yo Gresye, Dronne tonbe anba Lavil, Plizyè Bandi viktim, Bandi fini ak Machan !
▶︎

Lapolis frape Bandi yo Gresye, Dronne tonbe anba Lavil, Plizyè Bandi viktim, Bandi fini ak Machan !

#live :  PPP as a Strategic Financing Engine for FYDP IV and Tanzania Vision 2050.
▶︎

#live : PPP as a Strategic Financing Engine for FYDP IV and Tanzania Vision 2050.