BILIONI 2.99 ZATOLEWA GEITA MANISPAA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU - 1
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Hashim Komba amekabidhi hundi ya mfano ya Shilingi Bilioni 2.99 kwa vikundi 231 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Geita. Hafla hiyo ya utoaji mikopo imefanyika Novemba 19, 2025 katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan vilivyopo katika Kata ya Bombambili na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wanufaika wa mikopo hiyo. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa hafla hiyo, Mhe. Komba ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyokuwa na riba. Aidha, amewataka wanufaika kuhakikisha fedha hizo zinatumika katika shughuli za kiuchumi na sio kwa matumizi yasiyo na tija, huku akisisitiza ulazima wa kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili wengine waweze kunufaika. Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Ndg. Yefred Myenzi, amesema kwa awamu hii Manispaa ilitenga Bilioni 3.1 na vikundi vyote vilivyoomba mikopo na vyenye sifa vimeweza kupatiwa kiasi cha Bilioni 2.99 na vile ambavyo havikuwa na sifa vimeelekezwa kuboresha changamoto zilizopo ili awamu inayofata viweze kuomba vikiwa na sifa. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mikopo ya asilimia 10 ngazi ya Wilaya, Bi. Lucy Beda, amesema vikundi vyote vilivyopata mikopo vilikidhi vigezo na vimepatiwa elimu ya ujasiriamali na namna bora ya kutumia na kurejesha mikopo hiyo na zoezi hilo linaendelea kwa awamu ili kuhakikisha makundi mengi zaidi yanahusishwa. Akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa shughuli za utoaji na usimamizi wa mikopo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa, Afisa Maendeleo ya Jamii, Bi. Mariam John amesema Vikundi vya Wanawake 123 vimepata mkopo wa shilingi 1,168,500,000/=, Vikundi vya Vijana 101 vimepata mkopo wa shilingi 1,785,000,000/= na Vikundi vya watu wenye Ulemavu 7 vimepata mkopo wa shilingi 44,000,000/=.

ULITUKANA WAKALENJIN UKATUITA WAUWAJI, 2027 TUTAKUFUNZA DAWA!Aldai MP hits Gachagua below the belt

Maajabu ya Kijiji cha Lwamgasa, Ufahari wa Dhahabu na Mapinduzi ya Hexad

DIWANI AVULIWA UANACHAMA CCM KWA UTOVU WA NIDHAMU NA UKIUKWAJI WA KANUNI NA SHERIA ZA CHAMA GEITA.

Geita Wazipiku Simba na Yanga, Watengeneza Uwanja Mpya Kama Ulaya

THE HOUSEMAIDS AUDITION | MR MACARONI | MUMMY WA | PRETTY PLAY | TRINITY UGONABO | SOPHIE

BMG TV: Twenzetu mkoani Geita

Makala Maalum ya Vijana Manispaa ya Geita

RC SHIGELA AKAGUA MRADI WA BARABARA NA SHULE, ATOA MAELEKEZO KWA MKANDARASI - 2

WASIRA ATUA GEITA ATEMA CHECHE AWAONYA WANAOIBEZA CCM

Mr Speaker Sir ARRESTED Faces KSh 41M Charges Babu Owino Saves Him | plug Tv Kenya

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKIFUNGUA RASMI MAONESHO YA 8 YA TEKNOLOJIA YA MADINI MKOANI GEITA

HECHE: MKE WA TUNDU LISSU NA DADA YAKE POLE POLE WAMEUWASHA MOTO BUNGE LA ULAYA

A Side of Jamaica The Media Won't Show You!

GEITA-WASIRA AMCHANA MAKAVU TUNDU LISSU ‘WENJE NITAENDA KUMJIBU KWAO TARIME’

PROF. SHEMDOE AIPONGEZA MANISPAA YA GEITA KWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO @owm-tamisemi @ayo

MSUKUMA AWASILI KUCHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA GEITA

BREAKING: Ruto in Shock After Sifuna Unite in ODM Party | Boniface's Dream, Rogers Kakasungura

Fear grips Uasin Gishu as KWS hunts two giant pythons

Jionee uzuri wa Mkoa wa GEITA

