Kipimo cha kutisha, mja mzito achanganywa na matokeo ya HIV

Familia moja huko Diani kaunti ya Kwale imelaumu madaktari katika kituo kimoja cha kutoa huduma za afya kwa umma kwa kuhusika katika tukio la kutatanisha ambapo walimpima mwanamke mja mzito na kumpata ana virusi vya ukimwi, lakini miezi michache baadaye vipimo vikaonyesha kuwa hana virusi hivyo. Ni kisa ambacho nusura kisambaratishe familia, mbali na kuathiri afya ya mama na mtoto. Peter Mwangangi anaangazia kisa hiki ambacho kinazua maswali kuhusu suala zima la upimaji virusi vya ukimwi Watch more NTV Kenya videos at ntv.co.ke and nation.co.ke. Follow @ntvkenya on Twitter and like our page on Facebook: NTV Kenya.