MBUNGE MAFUWE AIBUA KERO YA UCHELEWESHAJI WA UHAMISHO KWA WALIMU NA WATUMISHI
Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe, leo ameibua hoja nzito kuhusu ucheleweshaji wa uhamisho kwa walimu na watumishi wengine wa umma, akisema hali hiyo imekuwa kero kubwa kwa watumishi wanaokamilisha taratibu zote lakini wanacheleweshwa kuhamishwa kutoka vituo vya kazi. Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bungeni jijini Dodoma, Mafuwe alieleza kuwa kuna walimu na watumishi waliomaliza mchakato wa uhamisho kwa mujibu wa taratibu, lakini wanabaki kwenye vituo vyao kwa miezi au hata miaka wakisubiri majibu yasiyo na uhakika. “Mtumishi anakuwa ameshamaliza kila kitu, lakini anabaki tu kwenye kituo akisubiri majibu. Hili ni jambo linaloumiza na linapaswa kushughulikiwa kwa haraka,” alisema Mafuwe. Katika majibu yake, Serikali kupitia Ofisi ya Rais - Utumishi na Utawala Bora, ilieleza kuwa mfumo wa sasa wa uhamisho kwa walimu na watumishi wengine wa umma kupitia Electronic Complaints and Compliments (ECC) umeshafanyiwa maboresho ili kuharakisha uamuzi wa uhamisho. “Katika mfumo wa ECC, ikiwa mtumishi ameomba uhamisho na msimamizi wake (supervisor) hatatoa majibu ndani ya muda, ombi hilo sasa litapelekwa moja kwa moja kwenye ngazi ya juu kwa ajili ya uamuzi,” ilieleza Serikali. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa maombi ya uhamisho hayatokwama kwenye ngazi ya wakuu wa vituo au waajiri wa moja kwa moja, hali ambayo imekuwa ikichangia malalamiko ya kucheleweshwa kwa watumishi katika kupata majibu. Wadau wa elimu na utumishi wamepongeza hatua hiyo ya serikali, wakisema itasaidia kupunguza msongamano wa maombi na kurudisha ari ya watumishi waliokuwa wakikata tamaa kutokana na kucheleweshwa kwa majibu ya uhamisho bila sababu za msingi. Mwisho

Kilio cha Uhamisho kwa Wafanyakazi wa Serikali Chamfikia Simbachawene, Ataka Busara Itumike.

VIDEO YA NAMNA YA KUSIJAJILI NA KUTUMIA MFUMO WA UHAMISHO

SIMBACHAWENE: WALIOTENGENEZA BARUA FEKI ZA UHAMISHO YUPO KIJANA WANGU

TAMISEMI LEO:KIMEUMANA WALIMU WALIOGUSHI UHAMISHO KUKIONA.. Dr Msonde

MHE. NDEJEMBI AKEMEA TABIA YA WAAJIRI SERIKALINI KUFICHA BARUA ZA UHAMISHO WA WATUMISHI WA UMMA

KATIBU MKUU UTUMISHI ATOA NENO KWA WANAOCHELEWA KUWAPOKEA WATUMISHI WAPYA

TAMISEMI LEO :TUMIENI MFUMO UHAMISHO WA WATUMISHI |UHAMISHO WA WALIMU 2024

LEAKED: The State House Trap Gachagua Dodged During Gen Z Protests | Lee Makwiny

Watumishi waliohama Vituo vya kazi kabla ya miaka 3 kurejeshwa walikopangiwa

Uhamisho wa watumishi sasa kutolewa kila Robo Mwaka - Serikali

MHE. SIMBACHAWENE AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUJIEPUSHA NA UHAMISHO USIOZINGATIA TARATIBU

MAELEKEZO YA KATIBU MKUU-UTUMISHI KWA WASIMAMIZI WA UTAWALA NA RASILIMALIWATU SERIKALINI

How US Air Force B 52 Pilot Performed an Emergency Takeoff at Full Speed

MAELEKEZO YA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA YA UHAMISHO KWENYE DIRISHA LA WATUMISHI PORTAL

Serikali yawaonya wanaoghushi uhamisho

Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe, rasmi akabidhiwa Ofisi na Eng. Joseph Nyamhanga

Uhamisho/Uhakiki/Malimbikizo ya Mishahara kulipwa/Promosheni/Maafisa utumishi /CWT hongereni

ኢትዮጵያ የምትመክርባቸው 8 አጀንዳዎች ይፋ ሆኑ | National Dialogue | ETV | EBC | EBCDOTSTREAM

E - UHAMISHO (ESS)_UHAMISHO WA KUBADILISHANA

