π—‘π—œπ— π—₯ 𝗬𝗔𝗧𝗒𝗔 π— π—”π—§π—’π—žπ—˜π—’ 𝗬𝗔 π—¨π—§π—”π—™π—œπ—§π—œ 𝗠π—ͺπ—˜π—Ÿπ—˜π—žπ—˜π—’ 𝗠𝗣𝗬𝗔 π——π—›π—œπ——π—œ 𝗬𝗔 π— π—”π—šπ—’π—‘π—π—ͺ𝗔 𝗬𝗔 π— π—Ÿπ—œπ—£π—¨π—žπ—’ π—¬π—”π—‘π—”π—¬π—’π—¦π—”π—•π—”π—•π—œπ—¦π—›π—ͺ𝗔 𝗑𝗔 π—ͺ𝗔𝗗𝗨𝗗𝗨

Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), tarehe 26 Februari 2026, kupitia mradi wa RAFT (Resilience Against Future Threats through Vector Control), imewasilisha matokeo ya utafiti kuhusu magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu pamoja na usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu, hatua inayolenga kuimarisha ustahimilivu wa taifa katika kukabiliana na vitisho vya magonjwa hayo. Akifungua kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIMR, Mkurugenzi wa Kuratibu na Kukuza Tafiti, Dkt. Nyanda Elias Ntinginya, amesema Tanzania inahitaji kuimarisha mifumo yake ya ufuatiliaji na maandalizi ili kukabiliana kwa ufanisi na ongezeko la vitisho vya magonjwa yanayoenezwa na mbu. Amesisitiza kuwa tafiti za kisayansi zinapaswa kuwa msingi wa maamuzi ya kisera, hasa katika kipindi hiki ambacho mabadiliko ya mazingira, ukuaji wa miji na ongezeko la mwingiliano wa watu vinaongeza hatari ya milipuko ya magonjwa kama dengue na magonjwa mengine ya virusi yanayoenezwa na mbu. Kwa upande wake, Mtafiti Kiongozi wa Mradi wa RAFT, Dkt. Alphaxard Manjurano, amesema lengo la mkutano huo lilikuwa kuwasilisha matokeo muhimu kuhusu usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu na vitisho vya magonjwa ya mlipuko yanayoenezwa na mbu, pamoja na kuyajadili kwa kina na wadau wakuu wa udhibiti wa wadudu dhurifu nchini. Akiwasilisha matokeo ya tathmini ya kitaifa ya utayari wa mfumo wa afya kukabiliana na vitisho vya mbu, Dkt. Manjurano alibainisha kuwa licha ya kuwepo kwa vituo 34 vya ufuatiliaji wa malaria (sentinel sites), bado kuna haja ya kuanzisha programu mahsusi ya kitaifa ya ufuatiliaji wa kawaida wa mbu wanaoeneza magonjwa. β€œKwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2024, ufuatiliaji wa mbu wa kuanzia hatua za mabuu hadi mbu waliokomaa haujawahi kufanyika kwa mfumo wa kitaifa. Hii inaonesha umuhimu wa kuimarisha mfumo wa utambuzi wa mapema wa hatari za milipuko ya magonjwa ya yanayoenezwa na wadudu,” alisisitiza Dkt. Manjurano. Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya kupitia Programu ya Taifa ya Udhibiti wa Malaria, Bw. Winfred Mwafongo, amesema matokeo hayo yatasaidia kuboresha sera na miongozo ya kukabiliana na malaria na magonjwa mengine yanayoenezwa na wadudu. Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Jovin Kitau, ameipongeza NIMR kwa kufanya utafiti huo, akisema utachangia kuimarisha kinga ya jamii dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu na kuongeza usalama wa afya ya umma. Aidha, Mtafiti Mkuu kutoka NIMR, Dkt. William Kisinza, amesema katika majadiliano ya kikao hicho wadau wamependekeza kuimarishwa kwa programu maalumu inayosimamia masuala ya wadudu dhurifu ili kuongeza ufanisi wa udhibiti wa magonjwa yanayoenezwa na wadudu. Kwa upande wake, Bi. Jackeline Martin, Mtafiti kutoka NIMR aliyefanya utafiti kuhusu ufanisi wa viuatilifu vilivyopo kwenye vyandarua, amesema matokeo yanaonesha ongezeko la usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu hivyo, jambo linaloonesha umuhimu wa kuendelea kuboresha mikakati ya udhibiti ili kuhakikisha vyandarua vinaendelea kuwa na ufanisi. Mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Protea, jijini Dar es Salaam, uliwakutanisha wadau mbalimbali wa udhibiti wa wadudu dhurifu kutoka Wizara ya Afya, NIMR, Shirika la Afya Duniani (WHO), Taasisi ya Afya ya Ifakara, pamoja na wadau wengine wa sekta ya afya.

NIMR YAONGOZA MDAHALO WA SERA ILI USHAHIDI WA KISAYANSI UTUMIKA KUKABILI MILIPUKO YA MAGONJWA
β–ΆοΈŽ

NIMR YAONGOZA MDAHALO WA SERA ILI USHAHIDI WA KISAYANSI UTUMIKA KUKABILI MILIPUKO YA MAGONJWA

33rd ANNUAL JOINT SCIENTIFIC CONFERENCE
β–ΆοΈŽ

33rd ANNUAL JOINT SCIENTIFIC CONFERENCE

UTAFITI - KUANGALIA MTAZAMO WA JAMII KUHUSU USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA KUDHIBIT WADUDU DHURIFU
β–ΆοΈŽ

UTAFITI - KUANGALIA MTAZAMO WA JAMII KUHUSU USHIRIKI WA WANAWAKE KATIKA KUDHIBIT WADUDU DHURIFU

FAHAMU NAMNA YA KUOMBA KIBALI CHA KUCHAPISHA MACHAPISHO YA UTAFITI NCHINI
β–ΆοΈŽ

FAHAMU NAMNA YA KUOMBA KIBALI CHA KUCHAPISHA MACHAPISHO YA UTAFITI NCHINI

π—‘π—œπ— π—₯ π—¬π—”π—­π—œπ—‘π——π—¨π—” π—¨π—§π—”π—™π—œπ—§π—œ π—¨π—§π—’π—”π—π—œ 𝗗𝗔π—ͺ𝗔 𝗬𝗔 π—žπ—œπ—–π—›π—’π—–π—›π—’ π—žπ—ͺ𝗔 π—ͺ𝗔𝗧𝗒𝗧𝗒 π—–π—›π—œπ—‘π—œ 𝗬𝗔 π— π—œπ—”π—žπ—” 5 π—žπ—¨π—£π—œπ—§π—œπ—” 𝗠π—₯π—”π——π—œ π—ͺ𝗔 π—¦π—§π—˜π—£π—£π—¦
β–ΆοΈŽ

π—‘π—œπ— π—₯ π—¬π—”π—­π—œπ—‘π——π—¨π—” π—¨π—§π—”π—™π—œπ—§π—œ π—¨π—§π—’π—”π—π—œ 𝗗𝗔π—ͺ𝗔 𝗬𝗔 π—žπ—œπ—–π—›π—’π—–π—›π—’ π—žπ—ͺ𝗔 π—ͺ𝗔𝗧𝗒𝗧𝗒 π—–π—›π—œπ—‘π—œ 𝗬𝗔 π— π—œπ—”π—žπ—” 5 π—žπ—¨π—£π—œπ—§π—œπ—” 𝗠π—₯π—”π——π—œ π—ͺ𝗔 π—¦π—§π—˜π—£π—£π—¦

NIMR INAVYOBORESHA HUDUMA ZA AFYA KUPITIA SHAHIDI ZA KISAYANSI
β–ΆοΈŽ

NIMR INAVYOBORESHA HUDUMA ZA AFYA KUPITIA SHAHIDI ZA KISAYANSI

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA KATAVI WAKUMBUSHWA WAJIBU WA KULINDA MALI ZA SERIKALI.
β–ΆοΈŽ

VIONGOZI WA TAASISI ZA UMMA KATAVI WAKUMBUSHWA WAJIBU WA KULINDA MALI ZA SERIKALI.

Nigeria: β€˜Renewed Hope’ or β€˜Hopelessness’? | Mehdi Hasan and Daniel Bwala | Head to Head
β–ΆοΈŽ

Nigeria: β€˜Renewed Hope’ or β€˜Hopelessness’? | Mehdi Hasan and Daniel Bwala | Head to Head

Rethinking climate justice
β–ΆοΈŽ

Rethinking climate justice

NCC YAFUNZA MBINU BORA ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UJENZI
β–ΆοΈŽ

NCC YAFUNZA MBINU BORA ZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UJENZI

Rwanda, M23 and the conflict in Congo explained | Start Here
β–ΆοΈŽ

Rwanda, M23 and the conflict in Congo explained | Start Here

MCHANGO WA KITENGO CHA TEHAMA KATIKA SHUGHULI ZA UTAFITI NIMR
β–ΆοΈŽ

MCHANGO WA KITENGO CHA TEHAMA KATIKA SHUGHULI ZA UTAFITI NIMR

June 2026 - Environmental
β–ΆοΈŽ

June 2026 - Environmental

WAHASIBU NA WAKAGUZI WAPEWA ELIMU YA JUU YA MAJUKUMU YA BODI YA BIMA YA AMANA.
β–ΆοΈŽ

WAHASIBU NA WAKAGUZI WAPEWA ELIMU YA JUU YA MAJUKUMU YA BODI YA BIMA YA AMANA.

KONGAMANO LA 33 LA KISAYANSI LA NIMR JUNI 9 2026
β–ΆοΈŽ

KONGAMANO LA 33 LA KISAYANSI LA NIMR JUNI 9 2026

END FUND PROJECT
β–ΆοΈŽ

END FUND PROJECT

Mahakama ya Rufani ya Tanzania  kuanza vikao vyake zanzibar
β–ΆοΈŽ

Mahakama ya Rufani ya Tanzania kuanza vikao vyake zanzibar

FAHAMU KUHUSU KITUO KIDOGO CHA UTAFITI CHA NIMR AMANI HILL
β–ΆοΈŽ

FAHAMU KUHUSU KITUO KIDOGO CHA UTAFITI CHA NIMR AMANI HILL

Raptors Reintroduction and Reinforcement Programmes: Experiences from the Field (Webinar)
β–ΆοΈŽ

Raptors Reintroduction and Reinforcement Programmes: Experiences from the Field (Webinar)

DC MYINGA  AHIMIZA TAASISI YA FEDHA YA BRAC KUJENGA TASWIRA CHANYA KWA JAMII.
β–ΆοΈŽ

DC MYINGA AHIMIZA TAASISI YA FEDHA YA BRAC KUJENGA TASWIRA CHANYA KWA JAMII.