KULIKONI IKULU ZANZIBAR CHAPCHAP KIKAO CHA VIONGOZI WAKUU NA WAJUMBE WA BARAZA LA ULAMAA ZANZIBAR

Zanzibar, 23 Ogasti, 2024 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Al hajj Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuna haja kwa Serikali kuangalia kwa karibu miundombinu duni ya madrasa, maslahi ya walimu wa madrasa na maimamu wa misikitini. Al hajj Dk. Mwinyi, aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar kwenye mazungumzo na viongozi wakuu na wajumbe wa Baraza la Ulamaa Zanzibar waliofika kumtembelea. Amesema, miundombinu ya madrsara, maslahi ya walimu madrsara na ma imamu wa misikitini nchini ni dhaifu mno, alisema ni vyema Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya kidini kuangalia njia nzuri ya kufanyakazi na kusaidia namna ya kuzitatua changamoto hizo. Akizungumzia suala la mmong’onyoko wa maadili kwa jamii, Al haj Dk. Mwinyi alisifu juhudi za Baraza hilo kwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii licha ya tatizo hilo kuwa kubwa. Pia, Alhaj Dk. Mwinyi ameupongeza uongozi na wajumbe wa baraza hilo kwa jitihada zao za kutoa elimu ya ndoa kwa wanandoa na warajis wa ndoa kwa Unguja na Pemba ili kupunguza matatizo na migogoro ya ndoa kwenye jamii sambamba na kutoa fatwa kutokana na changamozo zinazo ikabili jamii. Kuhusu migogoro mbalimbali inayohusiana na dini ya kiislamu kwenye jamii, Alhaj Dk. Mwinyi amelipongeza Baraza hilo kwa weledi wa utatuzi mzuri wa migogoro hiyo, sambamba na kutatua hata viashiria vinavyosababisha migogoro hiyo. Vilevile, Alhaj Dk. Mwinyi hakuacha kulisihi Baraza hilo kuendelea kuisimamia amani na utulivu kwa kutumia lugha moja kupitia viongozi wao, maimamu misikitini pamoja na wanasiasa kwenye majukwaa yao ili kuendeleza taifa lenye umoja na mshikamano. Naye, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaab, alipongeza juhudi za maendeleo anazozisimamia Alhaj Dk. Mwinyi hasa kwa kipindi kifupi cha uongozi wake, pia alimuahidi Al haj Dk. Mwinyi kumpa ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa baraza hilo kupitia misingi ya quran, hadithi, fikhi na tafsiri pamoja na kufuata miongozo na sunnah za Mtume (S.A.W) hasa kwenye suala zima la kusimamia ustawi, amani na utulivu wa nchi. Mapema, akizungumza kwenye kikao hicho, Katibu Mtendaji kutoka Ofisi ya Mufti Zanzibar, Sheikh Khalid Ali Mfaume amesema, miongoni mwa kazi za bara hilo mbali na kumshauri na kumsaidia Mufti mkuu wa Zanzibar pia wanatoa elimu kwa walimu wa madrasa, wanandoa na warajis wa ndoa kwa kuwakabidhi vibali baada ya kuhitimu mafuzo, kutatua mambo mbalimbali ya dini ikiwemo kutoa fatwaa kwa matatizo yanayoikabili jamii. IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR.

CCM Zanzibar hawauonei wivu Uzanzibari wao - Omar Said Shaaban | GUMZO MAALUM
▶︎

CCM Zanzibar hawauonei wivu Uzanzibari wao - Omar Said Shaaban | GUMZO MAALUM

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID
▶︎

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID

KADA wa CCM AJILIPUA - "RAIS SAMIA MUACHIE TUNDU LISSU - INATIA DOA UONGOZI WAKO BORA"...
▶︎

KADA wa CCM AJILIPUA - "RAIS SAMIA MUACHIE TUNDU LISSU - INATIA DOA UONGOZI WAKO BORA"...

DK.MWINYI APOKELEWA KWA SHANGWE NA WAFANYAKAZI WAKE IKULU - PEMBA.
▶︎

DK.MWINYI APOKELEWA KWA SHANGWE NA WAFANYAKAZI WAKE IKULU - PEMBA.

Heche Amshukia Patrobasi Katambi Kufungia Mikutano: 'Hauna Mamlaka Hayo'
▶︎

Heche Amshukia Patrobasi Katambi Kufungia Mikutano: 'Hauna Mamlaka Hayo'

Mufti Bara na Mufti Visiwani waenda Tabligh na Rais Husayn Mwinyi In shaa Allah
▶︎

Mufti Bara na Mufti Visiwani waenda Tabligh na Rais Husayn Mwinyi In shaa Allah

AHUKUMIWA MIAKA 20 - ALIYE MCHARANGA VISU MKE MWENZIE
▶︎

AHUKUMIWA MIAKA 20 - ALIYE MCHARANGA VISU MKE MWENZIE

LIVE: Trump arrives for dinner hosted by Macron at the Palace of Versailles
▶︎

LIVE: Trump arrives for dinner hosted by Macron at the Palace of Versailles

LIVE: SWEARING-IN CEREMONY OF NEW DISTRICT OFFICERS OF ZANZIBAR. ZANZIBAR HEADQUARTERS
▶︎

LIVE: SWEARING-IN CEREMONY OF NEW DISTRICT OFFICERS OF ZANZIBAR. ZANZIBAR HEADQUARTERS

📺🔴: ZEC YATANGAZA MATOKEO YA URAIS 2025 || UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR
▶︎

📺🔴: ZEC YATANGAZA MATOKEO YA URAIS 2025 || UCHAGUZI MKUU ZANZIBAR

ACT WAFUNGUKA AJIRA ZA WAZANZIBAR, WATAKA VIJANA KUPEWA KIPAUMBELE! 🔥
▶︎

ACT WAFUNGUKA AJIRA ZA WAZANZIBAR, WATAKA VIJANA KUPEWA KIPAUMBELE! 🔥

OMO NA JUSSA SEMENI MTAIFANYIA NINI ZANZIBAR, SIO KUPIGA KELELE ZISIZOELEWEKA: KATIBU MBETO
▶︎

OMO NA JUSSA SEMENI MTAIFANYIA NINI ZANZIBAR, SIO KUPIGA KELELE ZISIZOELEWEKA: KATIBU MBETO

RAIS MWINYI AWANANGA WAPINZANI , AWAJIBU KISOMI KUHUSU DENI LA ZANZIBAR "WAACHE UNAFIKI "
▶︎

RAIS MWINYI AWANANGA WAPINZANI , AWAJIBU KISOMI KUHUSU DENI LA ZANZIBAR "WAACHE UNAFIKI "

"Tulitumiliwa" anasema Katibu Mkuu wa Kwanza wa BLM juu ya Zanzibar kuingia kwenye Muungano
▶︎

"Tulitumiliwa" anasema Katibu Mkuu wa Kwanza wa BLM juu ya Zanzibar kuingia kwenye Muungano

Inside little Mogadishu in Uganda, Somalis City Away From Somalia 🇸🇴
▶︎

Inside little Mogadishu in Uganda, Somalis City Away From Somalia 🇸🇴

Zanzibar si ya kupitwa na Mauritius - OMO | Gumzo la Leo
▶︎

Zanzibar si ya kupitwa na Mauritius - OMO | Gumzo la Leo

#live:RAIS DKT.MWINYI AKIVUNJA BARAZA LA WAWAKILISHI LEO TAREHE 23, JUNI 2025
▶︎

#live:RAIS DKT.MWINYI AKIVUNJA BARAZA LA WAWAKILISHI LEO TAREHE 23, JUNI 2025

Mwanasheria Mkuu CHADEMA amjibu waziri Katambi zuio la Mikutano vyama vya siasa.
▶︎

Mwanasheria Mkuu CHADEMA amjibu waziri Katambi zuio la Mikutano vyama vya siasa.

#LIVE: Kuapishwa kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman
▶︎

#LIVE: Kuapishwa kwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman

Most Cheap Street food in Afghanistan | Kabuli pulao, Roasted Chicken, Biryani recipe, Punjabi Curry
▶︎

Most Cheap Street food in Afghanistan | Kabuli pulao, Roasted Chicken, Biryani recipe, Punjabi Curry