"DKT MWINYI AFICHUA MKAKATI MPYA: TATIZO LA MAJI ZANZIBAR LINAENDA KUISHA!"
Ikulu ZANZIBAR - 15 JULAI 2026. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amesema serikali inaendelea na mikakati mbalimbali kuhakikisha inailimaliza tatizo la ukosefu wa maji katika mikoa yote na kuwa na uhakika wa upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi . Rais Dkt Mwinyi Ameyasema hayo leo tarehe 15 julai 2026 alipokutana Waziri ya Maji Nishati na Madini Mhe Nadir Abdullatif na ujumbe wa Wizara ya Maji Nishati ya jamhuri ya muungano wa Tanzania uliongozwa na waziri wa wizara hiyo mhe juma awesu waliofika ikulu zanzibar kuonana na Rais Dkt Mwinyi . Amesema kuwa baadhi ya mikoa tayari imeshapata uwekezaji na kujengwa kwa miradi mikubwa katika maeneo hayo ili kuondosha usumbufu unawakumba wananchi wa kutafuta maji safi na salama ameitaja mikoa hiyo kuwa ni mkoa wa kaskazini unguja mkoa wa ,kusini na mkoa wa mjini magharibi ambayo tayari imeshapata uwekezaji . Rais Dkt Mwinyi Amesema sekta ya maji ni muhimu kwa maendeleo na ustawi wa jamii ambapo kwa sasa miradi mbali mbali inaendelea kujengwa katika maeneo mengi ya Zanzibar lengio ni kuhakikisha huduma hiyo inapatikana kwa urahisi na uhakika wakati wowote na kuondolea usumbufu wananchi . Aidha Dkt. Mwinyi ameishauri Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar kujifunza kupitia wizara ya maji nishati ya jamhuri ya muungano katika kusimamia na kutekeleza kwa ufanisi miradi ya maji hapa nchini , Amesema suala la teknoljia ni suala muhimu hivyo ni vyema kwa wizara hiyo kwenda na wakati ili kufanikisha miradi ya maji . Dkt Mwinyi ameipongeza Wizara ya Maji Nishati Zanzibar kwa kuja na mawazo ya miradi mikubwa ya maji ambayo itaondoa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama katika mikoa yote . Naye Waziri wa Maji jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Juma Awesu amempongeza Dkt Mwinyi kwa utekelezaji wa miradi mbali mbali ya kimaendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuahidi kwa wizara hiyo kutoa ushirikiano mkubwa kufanikisha miradi hiyo ambayo ina umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Zanzibar . Aidha amesea kuwa izara hiyo tayari imeshaandaa mfumo maalum wa matumizi ya teknolojia utakaosaidia wananchi kutoa taarifa na kuondoa changamoto kwa wananchi katika upatikanaji wa huduma ya maji .

MWENEZI WA CCM ZANZIBAR AMJIBU OTHMANI MASOUD KWA KINACHOENDELEA HIVI SASA

🔴#LIVE:: OMO WA ACT WAZALENDO BADO ASHIKILIA PALE PALE AIZUGUUKA PEMBA AKITETA NA WANANCHAMA -

@vugaonlinetv: Mhe OTHMAN MASOUD AFAFANUA MAMBO YALIO SAINIWA NA NAIBU KATIBU MKUU ZANZIBAR

WAZIRI NADIR: KAMPUNI ZISIZOKAMILISHA MIRADI YA UMEME KWA WAKATI ZITACHUKULIWA HATUA

DKT MWINYI AIKARIBISHA SWEDEN KUONGEZA UWEKEZAJI ZANZIBAR, AIPONGEZA KWA MSAADA WA MAENDELEO

Zanzibar maeneo ya Vuga Mnazimmoja Maisara Migombani Mbweni na Chukwani July 2026 @discoverzanzibar

Sio mwanamke! Huu ndio ukweli kuhusu kuondolewa kwa Sheikh Alwalid katika nafasi ya Sheikh wa Mkoa.

"OTHMAN MASOUD AFUNGUKA MAZITO: 'MARIDHIANO SI YA ACT WALA CCM, NI YA WAZANZIBARI WOTE'"

ALLY KAMWE ATOA TAARIFA USAJILI WA FEISAL NA AZIZ KI/KOCHA MPYA AMEANZA NAO/ WACHEZAJI HAWA KUACHWA

"HEMED AKAZA KAMBA! AWAONYA WAKANDARASI WANAOCHELEWESHA MIRADI YA MAENDELEO ZANZIBAR"

DR SULLEH AWEKA WAZI SABABU ZA SHEIKH WALID KUSIMAMISHWA/MTOTO WAKE APIMWE DNA/WALID NI SHEIKH BORA

MAHOJIANO: KOMREDI MBETO AELEZA KINACHOENDELEA BAADA YA TAMKO LA MARIDHIANO ZANZIBAR

SGR KIGOMA UJENZI UNAENDELEA

MARIDHIAYANO HALITETE CUF WAINGILIA KATI MAZITO YAFICHUKA MAALIM SEIF AHUSISHWA

Ni dhamira njema pekee itakayoyadumisha makubaliano haya - OMO | GUMZO LA MARIDHIANO

OMO AKATA SHAURI KUWAJIBU KUHUSU MARIDHIANO YA ZANZIBAR

DALILA ATELEKEZWA DAR AKIWA NA WATOTO 5 NA MTU ALIYEMTOA ZANZIBAR ILI KUMSAIDIA

KUMEKUCHA! KITWANA ATAKA VIONGOZI WAACHE OFISINI, WASHUKE KUSIKILIZA WANANCHI

WANACHAMA 200 WA CUF PEMBA WAHAMA CHAMA, WATAJA SABABU LUKIKI ZA UAMUZI HUO

