ONYO Hili RAIS MWINYI AMEKUTANA NA UJUMBE WA MASUALA YA NISHATI KUTOKA OMAN IKULU ZANZIBAR
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema miradi ya kimkakati inayoendeshwa Zanzibar inahitaji kuzingatia wakati katika utekelezaji wake ili kuleta tija kwa Taifa. Rais Dk. Mwinyi ameeleza hayo Ikulu, Zanzibar alipokutana na Ujumbe wa watendaji kutoka Kituo cha Nishati cha Oman uliofika kuelezea hatua za miradi wanayoisimamia hapa Zanzibar ukiwemo miradi ya Maji, Nishati na ukarabati wa Mji Mkongwe ambao ni urithi wa dunia. Rais Dk. Mwinyi ameuhakikishia ujumbe huo kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itawapa ushirikiano wa hali ya juu ili kufanikisha miradi hiyo aliyoielezea kuwa na umuhimu mkubwa kwa Uchumi wa Zanzibar, maendeleo na ustawi wa wananchi wake. Dk. Mwinyi ameueleza Ujumbe huo kutosita kuwasilisha Serikalini vikwanzo na changamoto zozote zitakazojitokeza kwenye utekelezaji wa miradi hiyo ili Serikali ichukue hatua za haraka kukabiliana nazo. Akitilia mkazo mradi wa maji safi na salama Rais Dk. Mwinyi ameushauri ujumbe huo kuweka mazingatio zaidi kwa kuhakikiksha upatikanaji wa maji ya uhakika kwa maeneo yote yaliyopitiwa na miradi yao. Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kufarajika kwake kwa muendelezo na utayari wa utekelezaji wa miradi inayosimamiwa na kituo cha Nishati cha Oman hapa Zanzibar ambayo inaendelea kuimarisha ushirikiano na uhusiano wa kudumu baina ya Oman na Zanzibar. Naye, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kituo hicho, Abdallah Humaid Al Ma’amary alisema, moja ya maboresho ya Mji Mkonge ni kuufanya kuwa mji wa kisasa (Smart City) bila kuharibu uhalisia wa mji huo na kuzingatia vigezo na miongozo ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kuwa ni urithi wa dunia na kielelezo muhimu cha historia ya Zanzibar. Ameeleza kuwa tayari wamekamilisha upembuzi yakinifu kwa miradi wanayotarajia kuitekeleza na kusifu ushirikiano wanaoupata kutoka kwa watendaji wa kuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar waliopitiwa na miradi hiyo.

🔴TAARIFA YA HABARI YA ASUBUHI, JULAI 02, 2026

Summer Mix 2026 🍓 Best Popular Songs 2026 🍓Faded, Supergirl, A Sky Full Of Star, Perfect Cover love1

MRADI MKAKATI WA KIWANJA CHA NDEGE KISIWANI PEMBA#clamvevo #ikuluzanzibar #vuga #wasafimedia

Extreme heat warning: The News4 Rundown | NBC4 Washington

Zanzibar Ports Corporation (ZPC) hosts a delegation from the Singapore Business Federation.

UJENZI WA KITUO CHA UKAGUZI WA MAGARI MARUHUBI ZANZIBAR UKIENDELEA

OMO makes clear its position on land and rights of Zanzibari | ZANZIBAR DECIDES 2025

KAHAMA KIMENUKA! HAPI AIBANA CHADEMA KWA FEDHA ZA NJE 🔥

Local businesses sending supplies to Venezuela

KIMENUKA ZANZIBAR! ACT WAZALENDO YAPINGA KAULI ZA MAWAZIRI KUHUSU UZANZIBARI NA ZAN ID

Trump tours newly built Theodore Roosevelt Presidential Library in North Dakota

KALONZO: RUTO SCARED OF 2027

DEREVA WA JOHN HECHE AKUTWA AMEFARIKI LODGE

Relaxing Rain Sounds and Soft Piano Music for Deep Sleep, Stress Relief, and Peaceful Nights

Dkt. Lwaitama akosoa agizo la Waziri Katambi, Akemea mpasuko na Kutoa Ushauri kwa Taifa.

SECOND VICE PRESIDENT OF ZANZIBAR - INSPECTED THE CONSTRUCTION OF AFCON 2027 STADIUM - FUMBA

